logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wema Sepetu - sikutaka kukosana na mpenzi wangu ndio maana niliacha ulevi

Mwigizaji Wema Sepetu wa Tanzania asimulia maisha yake baada ya kuacha vileo.

image
na

Habari29 September 2023 - 05:12

Muhtasari


• Wema kwa miaka mingi amejihusisha na uingizaji wa filamu na kujizolea zawadi chungu nzima. 

 

Wema Sepetu azungumzia kuhusu mafanikio ya maisha yake

Mwigizaji mwenye wa filamu za Bongo  mwenye uzoefu Wema Abraham Sepetu amefunguka kuwa ana takribani  mwaka tangu aache kutumia vileo vya aina yoyote.

 Wema hakuficha furaha yake wakati wa kusherekea siku yake ya kuzaliwa baadaa ya waingizaji na wasanii maarufu kumtembelea.

Sherehe hii na ambayo ilifanyika nyumbani kwa muigizaji huyu ilihudhuriwa na wasanii wengi akiwemo Hamisa Mobbeto,Nandy,na Ruby.

Wema kwa miaka mingi amejihusisha na uingizaji wa filamu na kujizolea zawadi ghali. Aliongeza kuwa kwake siku ya kuzaliwa ndio siku muhimu sana maishani mwake.

 

'Nina furaha sana leo wengi wanashindwa kwa nini nimefanya sherehe ghali mna lakini kwangu mimi siku hii ni muhimu kuliko siku zote nimebarikiwa sana na wakati mtu anapozidi kuwa na umri mkubwa ndipo ana uwezo wa kusherekea zaidi"..

Muigizaji huyu alipozidi kuhojiwa na wanablogu alisimulia zaidi  cha muhimu kwa baada ya kukaa miezi kadhaa bila kutumia vileo.

"Kwa hakika watu  wengi akiwemo mamangu mzazi na mpenzi wangu walitaka niache pombe kwa muda mrefu jambo ambalo nafurahi sana kwa kweli najuta maisha niliokuwa nayo wakati nitumia pombe ila kwa sasa moyo wangu umejawa na amani kwa kuacha pombe .

Mara mingi tungetofautiana na mpenzi wangu kwa tabia zangu za pombe kwa niliona jambo hili linaweza kuleta mfurugano kwa kuwa mume wangu hapendi ulevi.

Wema alimsifu mumewe na marafiki kwa kufanikisha kwa kugharamikia vyakula na hata mapambo ya sehumu iliyotengwa kusherekea siku yake ya kuzaliwa.

 

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved