logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond ambwaga Burna Boy kushinda tuzo ya MTV EMA 2023

Pia ndiye msanii wa kwanza barani Afrika kufikisha watazamaji milioni 900 kwenye YouTube.

image
na Radio Jambo

Habari06 November 2023 - 07:10

Muhtasari


• Pia ndiye msanii wa kwanza barani Afrika kufikisha watazamaji milioni 900 kwenye YouTube.

• Hafla ya tuzo hizo ilifanyika katika ukumbi wa Paris Nord Villepinte, nchini Ufaransa.

Diamond Platnumz

Msanii wa kutoka Tanzania, Diamond Platnumz, amefanya urejeo wake kwenye tuzo z MTV EMA mwaka huu kuwa kubwa Zaidi baada ya kuwabwaga wasanii wakubwa barani Afrika kushinda tuzo hiyo kwa mara ya pili katika historia ya maisha yake ya muziki.

Katika tuzo hizo zilizotolewa usiku wa Jumapili, Diamond aliibuka kama msanii bora wa Afrika, Best African Act.

Katika kitengo hicho, Diamond alikuwa anamenyana na wasanii kama vile Burna Boy, Asake, wote kutoka Nigeria na mrembo chipukizi kutoka Cameroon, Libianca pamoja na Tyler ICU.

Diamond Platnumz aliwahi kushinda tuzo mbili za Msanii Bora wa Afrika na mwimbaji Bora Duniani (Afrika/India) kwa usiku mmoja kwenye MTV EMA 2015.

Pia ndiye msanii wa kwanza barani Afrika kufikisha watazamaji milioni 900 kwenye YouTube.

Hafla ya tuzo hizo ilifanyika katika ukumbi wa Paris Nord Villepinte, nchini Ufaransa.

Ili kutazama orodha kamili ya washindi wote, ifuate kwenye kiunganisho hiki cha tovuti rasmi ya MTV EMA.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved