logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tutarudi maandamano ikiwa mazungumzo yatatibuka - Martha Karua

Tunakataa vitisho na tunatoa wito , kuungana ili kurejesha hali tulivu katika taifa letu.

image
na

Habari16 November 2023 - 13:01

Muhtasari


• Karua alitoa wito kuondolewa kwa ushuru kwa asilimia 8 kwa mafuta ili kuleta utulivu wa gharama ya maisha.

Kiongozi wa NARC Kenya Martha Karua amesema kuwa wako tayari  kurejealea  maandamano  barabarani iwapo mazungumzo kati ya  Kenya Kwanza na muungano wa Azimio la Umoja yatatibuka. 

Karua aliwataka Wakenya kudai haki zao za kiraia, kisiasa na kibinadamu kikamilifu, akisema kwamba hata katika hali ya shida wakati wa maandamano, hawataathiri haki zao.

"Hata tukisafirishwa hadi mbinguni kwa kuauwa wakati wa maandamano, NARC Kenya na watu wa Kenya wanasema kwamba mazungumzo yakishindikana kwa sababu yanaonekana kushindwa, hatutaacha haki zetu, na tutarudi kwenye mitaa," alisema.

"Tunakataa vitisho na tunatoa wito kwa Wakenya kuungana na kushikana mikono ili kurejesha hali tulivu katika taifa letu," Karua aliongeza.

Akizungumza katika makao makuu ya chama cha NARC Kenya mnamo Alhamisi, Oktoba 16, Karua alitoa wito kuondolewa kwa ushuru wa asilimia 8 kwa mafuta ili kuleta utulivu wa gharama ya maisha.

 Pia alitoa wito wa kuchunguzwa upya kwa rekodi za viongozi waliochaguliwa, akiwataka wananchi kushiriki kikamilifu katika kubuni usimamizi wa masuala ya umma.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved