logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kipusa kufanya upasuaji kuondoa tumbo la uzazi akisema hataki kuzaa mtoto aje kufa

Mashabiki wake waligawanyika kwa maoni.

image
na Radio Jambo

Habari17 November 2023 - 10:06

Muhtasari


• "Sababu kuu ya kifo ni maisha yenyewe. Kwa hiyo ili kukomesha kifo, ni lazima mtu akomeshe uzazi" alisema.

Mrembo kufanya upasuaji kuondoa tumbo la uzazi

Mrembo Mwigizaji wa Nollywood, Etinosa Idemudia ametangaza kuwa hivi karibuni atafanyiwa upasuaji wa kutoa tumbo lake la uzazi.

Mama wa mtoto mmoja ambaye alifichua haya muda mfupi baada ya taarifa za ‘uongo’ za kufariki kwa mwanamuziki wa Nigeria Oladips kwenye mitandao ya kijamii alisema, "ili kukomesha kifo, ni lazima kukomesha uzazi."

"Sababu kuu ya kifo ni maisha yenyewe. Kwa hiyo ili kukomesha kifo, ni lazima mtu akomeshe uzazi. Kile ambacho hakijazaliwa hakitakufa kamwe. Hata mimi mwenyewe siko tayari kwa mazungumzo haya ya kina. Ni ya kina kuliko ninavyoweza kuelewa," aliandika kupitia X.

Akijibu maoni ya mtumiaji ambaye alikubaliana naye, Etinosa alisema angetoa tumbo lake, akibainisha kuwa hakuna mtoto wake ambaye atakuja duniani kusubiri kifo.

"Mungu akubariki. Sababu ninafanya upasuaji hivi karibuni ili kutoa tumbo langu. Hakuna mtoto wangu anayekuja katika ulimwengu huu kusubiri kifo,” alichapisha.

Mashabiki wake waligawanyika kwa maoni. Haya hapa ni baadhi ya maoni ya watu;

“Karibu sisi sote tuna maswali kuhusu maisha, kuteseka, kifo, na wakati ujao. Pia tunahangaikia mambo ya kila siku, kama vile kutafuta riziki au kuwa na familia yenye furaha, Maisha yalianzaje? Kwa nini tuko hapa? Kwa nini watu wasio na hatia wanateseka? Nini kinatokea mtu anapokufa?” aliuliza mdau.

“Huu ni uamuzi mzito sana wa kufanya, kumbuka kuwa huu hauwezi kutenduliwa, ukishamaliza ✅,Hakuna kurudi nyuma. Natumai hatajutia maisha haya ya baadaye,” mwingine alisema.

Maoni yako ni yepi?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved