logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Muigizaji Awinja afunguka baada kuji'surprise na gari la kifahari

kununua gari  ni mojawapo ya shukrani kwangu kwa kazi nzuri  ninayofanya  Awinja asema

image
na

Habari17 November 2023 - 08:00

Muhtasari


• Awinja alinunua gari la kifahari aina ya Jeep siku chache zilizopita akisema kuwa imekuwa ni ndoto yake ya muda mrefu.

Muigizaji Awinja

Muigizaji Jacky Vike almaarufu Awinja Nyamwalo amefunguka siku chache baada ya kununulia gari  aina ya 'Jeep Wrangler'  gari ambalo amesema amelitamani kwa muda mrefu.

Awinja alisema kuwa amewekeza kwa muda mrefu kununua gari hilo ili kutimiza ndoto yake kwani baadhi ya malengo yake ni kujirudishia shukrani  kwa bidii zake kuigiza.

"kufanikisha malengo yangu ya kujinunulia gari hilo la kifahari nimeweza kuekeza kwa muda mrefu ili kutimiza ndoto yangu, gari hilo aina ya Jeep limekuwa tamanio langu kwa magari yote kwa kuwa nilipata ufahamu wa kulijua zaidi kupitia marafiki wangu.

Kulingana na Awinja yeye hufanya kazi zake za uigizaji akiwa na matumaini kuwa kazi anazozifanya zitamletea mafanikio kwa maisha yake ili kujikimu kimaisha na pia kujirudishia shukrani kwa kujinunulia chochote ambacho ni tamanio la roho yake.

"Kuigiza ni jambo gumu zaidi ila mimi hujisatiti kuakikisha chochote naigiza kinaweza kuwa manufaa kwa maisha yangu,ndio maana najituma sana ili niweze kutimiza ndoto zangu na kujirudishia shukrani kwa vyovyote vile, kununua gari ilikuwa mojawapo ya shukrani kwangu kwa kazi nzuri.

 

 

 

 

Mchekeshaji Awinja

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved