logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Pasta aliyewalaghai waumini wa kanisa lake Ksh 213M ajitetea kuwa ni Mungu alimtuma

Alisema kwamba aliingia katika biashara ya cryptocurrency kwa sababu "Bwana" alimwambia

image
na Radio Jambo

Habari24 January 2024 - 09:18

Muhtasari


• Bw. Regalado alisema kuwa hataki wawekezaji kuwa na "wazimu" kwa waendesha mashtaka.

Mchungaji wa kanisa moja katika jimbo la Colorado nchini Marekani amewashangaza wengi baada ya kudai kwamba Mungu ndiye alimtuma kuwalaghai waumini wa kanisa lake Zaidi ya dola milioni 1.3 – sawa na milioni 213 za Kenya.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyowashangaza wengi kwenye jarida la The New York Times, pasta Eli Regalado na mke wake Kaitlyn walipandishwa mahakamani kwa dai la kuwauzia waumini wa kanisa lao hisa za biashara ya hela, INDXcoin kwa ahadi ya uwongo kwamba wawekezaji wanaonunua sarafu ya crypto watakuwa matajiri.

Hata hivyo kaitka kujitetea kwake, mchungaji huyo aliishangaza mahakama kwa vicheko baada ya kudai kwamba kila kitu ambacho alikifanya ni kufuata maagizo kutoka kwa Mungu.

Katika video iliyoonwa na jarida hilo akihutubia malalamiko hayo wiki jana, Bw. Regalado alisema kuwa hataki wawekezaji kuwa na "wazimu" kwa waendesha mashtaka.

"Lazima wafanye hivi," alisema. "Namaanisha, ikiwa unafikiria juu ya hili: Tuliuza sarafu ya siri bila njia ya kutoka wazi. Tulifanya. Tulimkubali Mungu kwa neno lake na tukauza sarafu ya siri bila njia ya kutoka wazi.”

Bw. Regalado alisema kuwa kwa sababu ya matatizo ya kubadilishana cryptocurrency, wawekezaji hawakuweza kuchukua fedha zao.

Bwana Regalado pia alisema kwenye video kwamba aliingia katika biashara ya cryptocurrency kwa sababu "Bwana" alimwambia.

Alisema kwamba wakati fulani Mungu alimjia ndoto na kumwomba afanye hivyo, naye akakubali kwamba yeye na mke wake walitumia pesa hizo katika “urekebishaji wa nyumba ambao Mungu alituambia tufanye.”

Ripoti hiyo pia ilimnukuu Bw. Regalado akisema bado ana matumaini kwamba wawekezaji wangeweza kurejeshewa pesa zao, na kwamba anaamini “Mungu atafanya muujiza katika sekta ya fedha.”


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved