logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakuna sheria nchini Kenya inayoharamisha mtu kuwa shoga - Seneta Edwin Sifuna (video)

“Hakuna sheria nchini Kenya dhidi ya kuwa mashoga. Sheria hiyo haipo; unaiunda tu." alisema.

image
na Radio Jambo

Habari01 February 2024 - 09:54

Muhtasari


• Seneta huyo aliweka wazi kwamba kilichopo ni kanuni ya adhabu inayoweka adhabu ya kufanya ngono ambayo ni kinyume na utaratibu wa asili.

Mgombea wa useneta wa Nairobi Edwin Sifuna wakati wa kibali Kasarani.

Seneta wa Nairobi ambaye pia ni katibu wa kitaifa wa chama cha upinzani cha ODM, Edwin Sifuna amezua utata miongoni mwa Wakenya baada ya kudai kwamba kufikia sasa hakuna sheria nchini Kenya inayoharamisha mtu yeyote kuchagua kuwa shoga au la.

Akizungumza katika runinga ya Citizen, seneta huyo aliweka wazi kwamba kilichopo ni kanuni ya adhabu inayoweka adhabu ya kufanya ngono ambayo ni kinyume na utaratibu wa asili, ikiwa ni pamoja na kati ya mwanamume na mwanamke.

“Hakuna sheria nchini Kenya dhidi ya kuwa mashoga. Sheria hiyo haipo; unaiunda tu. Kanuni ya adhabu inaweka adhabu ya kufanya ngono kinyume na utaratibu wa asili, ikiwa ni pamoja na kati ya mwanamume na mwanamke. Nchi hii, ubakaji wa kisheria unaitwa ndoa ya mapema," Sifuna alisema.

Tamko hili ambalo wengi wa Wakenya wamelichukua nje ya muktadha linakuja wakati ambapo viongozi wengi wakiongozwa na mke wa naibu rais, Mama Dorcas Gachagua ako katika mstari wa mbele kupinga ujio wa vitendo na visa vya ushoga, maarufu kama LGBTQ.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved