logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Musome Yohana 8:32- Maribe avunja kimya baada ya kuondolewa mashtaka

Maribe alieleza wanahabari nje ya mahakama Milimani kwamba hakuwa na mengi ya kusema.

image
na

Habari09 February 2024 - 11:27

Muhtasari


  • Maribe alieleza wanahabari nje ya mahakama Milimani kwamba hakuwa na mengi ya kusema. 
  • Maribe aliachiliwa Ijumaa juu ya ukosefu wa ushahidi.
akiwa katika Mahakama ya Milimani, mbele ya Hakimu Grace Nzioka mnamo Februari 9, 2024, wakati wa hukumu ya kesi ya mauaji ya mfanyabiashara Monica Kimani .

Mwanahabari Jacque Maribe amevunja kimya baada ya hakimu Grace Nzioka kumuondolea mashtaka ya mauaji ya Monica Kimani.

Maribe alieleza wanahabari nje ya mahakama Milimani kwamba hakuwa na mengi ya kusema. Hata hivyo alihimiza watu kuenda kusoma kitabu cha Yohana 8:32.

"Sihitaji kusema chochote lakini nitasema nenda kasome Yohana 8:32. Kwa maana mtafahamu kweli na hiyo kweli itawaweka huru. Asante," Maribe alisema.

Mtangazaji  wa zamani wa Citizen, Jacque amekua ndani na nje ya mahakama kwa miaka 5 iliyopita. Alikuwa mshtakiwa wa pili kwa kesi hiyo pamoja na mshtakiwa wa pili, Jowie Irungu.

Mwili wa Monica ulipatikana nyumbani mwake, Lamuria Gardens Apartment ambayo iko kando ya barabara ya Kitale, off Dennis Pritt, Kilimani.

Hata hivyo Maribe aliachiliwa Ijumaa juu ya ukosefu wa ushahidi. Katika hukumu yake, Hakimu Grace Nzioka alisema kuwa mashtaka dhidi ya Maribe haiukuwekwa vizuri.

"Ni maoni yangu kwamba shtaka lililoletwa dhidi ya mshtakiwa wa pili halikuwa shitaka sahihi", hakimu alisema.

" Matokeo yake ni kwamba upande wa mashtaka haukutoa ushahidi wa kutosha kwa mahakama yake kumpata mshtakiwa wa pili na hatia  ya kosa hilo. mauaji ya Monica Nyawira Kimani usiku wa Septemba 19,2018".

Jowie na Jacque wamekua kwenye kesi kuanzia 2018 na upande wa mashtaka kuita mashaidi 35.

Hakimu Nzioka amepata Jowie Irungu na hatia ya kuua Monica Kimani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved