logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond kwangu hatoki hata mmpe 'Sim 2' - Zuchu atuma taarifa kwa wanaotaka waachane (video)

Zuchu alisema ameachana na Diamond kisa kutendwa.

image
na Radio Jambo

Habari26 February 2024 - 05:44

Muhtasari


• Mwishoni mwa juma, Zuchu alikwenda kwenye Instagram na kuachia ujumbe mrefu akisema kwamba amechoka kutendwa katika mapenzi.

Mama Dangote akanusha Diamond kutoka kimapenzi na Zuchu.

Msanii wa kike kutoka lebo ya WCB Wasafi, Zuchu ametengua kauli yake ya siku mbili zilizopita kwamba wameshaachana na Diamond Platnumz na kuwa yuko single.

Akiwa katika shoo ya full moon party kisiwani Zanzibar pamoja na Diamond, Zuchu alisema kwamba yeye na Diamond ni kama mtoto mchanga na usingizi, kwani hawawezi kuachana leo wala kesho.

Picha na video ambazo zimesambazwa kutoka kwa tukio lao huko Zanzibar wikendi iliyopita zinawanyesha wawili hao wakiwa katika mikao ya mahaba mazito. Kinyume na kauli zao siku mbili zilizopita kwamba wameshatengana.

Zuchu wakati wa kutumbuiza kwake, aliamua kutoa taarifa kwa mahasidi wa penzi lao upande wa pili akiwaambia kwamba kama walikuwa wanakesha wakisubiri Diamond kutoka ubavuni mwake basi wataharibu mishumaa tu hadi kukuche.

“Ila wacha tutume taarifa kwa upande wa pili si ndio? Wanaohisi watamchukua [Diamond], nawaona mnamaliza Miungu, mnamaliza mikao na utundu, huyu kwangu hapa hatoki hata mmpe mkun**,” Zuchu aliimba.

Mwishoni mwa juma, Zuchu alikwenda kwenye Instagram na kuachia ujumbe mrefu akisema kwamba amechoka kutendwa katika mapenzi na ameshafikia hatua ya kuwa bila mpenzi.

“HABARI FAMILIA .ILIBIDI KUPOST HII ILI KUFUTA DHAMIRI YANGU. KUANZIA LEO HII MIMI NA NASIBU (DIAMOND) HATUKO PAMOJA,” Zuchu alitangaza kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Aliongeza, “NAJUA HILI LIMEKUWA JAMBO LETU LAKINI AS HARD AS IT IS KUMUACHA MTU UNAEMPENDA HII NAOMBA MUNGU IWE YA MWISHO NA NIANZE MAISHA MAPYA. MAPENZI NI HESHIMA KWA BAHATI MBAYA SANA HIKO KIMEKOSEKANA KWETU.”

Hii ni baada ya kuibuka kwa video ya Diamond na babymama wake Zari wakiwa wameshikana mikono wakitembea kwa mwendo wa taratibu, Diamond akimtaja Zari kama ‘dadangu’.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved