logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Embarambamba ni chaguo stahiki kwa Wakenya sababu hamthamini maudhui safi - Ezekiel Mutua

Natamani wasanii hawa wavue nguo na kutumbuiza kanisani hivyo - Mutua.

image
na Radio Jambo

Habari27 February 2024 - 08:11

Muhtasari


• "Hata hivyo, ninaamini kuwa Kenya inastahili Embarambara. Hatuthamini maudhui safi,” Mutua alisema kupitia Facebook.

Embarambamba.

Mkurugenzi mkuu wa halimashauri ya kusimamia hakimiliki za kazi za kisanaa nchini MCSK, Ezekiel Mutua amesema kwamba msanii wa injili mwenye vitimbi, Chris Embarambamba ni picha halisi ya kile ambacho Wakenya wengi wanashabiki.

Mutua ambaye aliwahi kuwa mkurugenzi katika bodi ya kutathmini ubora wa kazi za Sanaa, KFCB alisema kwamba amepata watu wengi wakimtaka kuingilia kati kumkomesha Embarambamba ambaye amekuwa akiachia nyimbo zenye maudhui chafu akijificha nyumba ya injili.

Hata hivyo, Mutua akiwajibu, alisema kwamba kwa vile Wakenya wengi wana hulka ya kuunga mkono maudhui chafu na kupuuza maudhui safi, basi Embarambamba anawafaa kabisa na hawafai kulalamika kwa vile anachokifanya ndicho kile wengi wanafurahia.

“Nimeona watu wakinitagi kwenye uwazimu wa Embarambara na mambo mengine kama hayo kwenye mitandao ya kijamii. Wakenya, mamlaka yangu si udhibiti tena. KFCB ni chombo kilichoidhinishwa na sheria kuhakiki na kuainisha maudhui. Hata hivyo, ninaamini kuwa Kenya inastahili Embarambara. Hatuthamini maudhui safi,” Mutua alisema kupitia Facebook.

Mkurugenzi huyo wa MCSK ambaye alifahamika Zaidi enzi za uongozi wake wa KFCB na misimamo yake mikali dhidi ya kazi zozote za Sanaa zenye maudhui ya kupotosha jamii aliilaumu jamii na kanisa pia kwa kupalilia maudhui chafu badala ya kuyakemea.

“Tunaonekana kutojali hata wakati yaliyomo ni ya kufuru. Makanisa na viongozi wa jumuiya huwa kimya wakati maudhui kama hayo yanapoongezeka. Natamani wasanii hawa wavue nguo na kutumbuiza kanisani hivyo hadi watupishe dhamiri!” aliongeza.

Baadhi ya Wakenya walimtaka Mutua kumkomesha Embarambamba muda mfupi baada ya msanii huyo kutoka Kisii kuachia kionjo cha wimbo wake ‘Tuko uchi mbele za Mungu’ akionekana kucheza densi bila nguo, Zaidi ya taulo pekee.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved