logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond ataja sababu zinazomzuia kuzungumzia kesi ya P Diddy

"Nilimheshimu kama msanii, na mtu ambaye katika muziki anajua vitu vingi sana,” Diamond alisema.

image
na Radio Jambo

Habari12 April 2024 - 07:01

Muhtasari


• P Diddy amekuwa chini ya uchunguzi kwa wiki kadhaa sasa baada ya watu mbalimbali kujitokeza na kudai kwamba amewahi wadhulumu kingono.

Gwiji wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz kwa mara ya kwanza amevunja kimya chake kuhusu kesi za unya yasaji wa kingono ambazo zinamuandama rapa wa Marekani, P Diddy.

 

Akizungumza na waandishi wa habari za burudani wakati wa kutangaza tamasha la muziki litakalofanyika baadae mwezi huu, Platnumz alisema kwamba P Diddy ni rafiki yake na kuna vitu vingi tu ambavyo vinamzuia kuzungumzia kesi hiyo ambayo imekuwa ikichunguzwa kwa muda sasa.

Diamond alikumbuka jinsi P Diddy aliwakaribisha nyumbani kwake miaka ya nyuma yeye na timu yake walipokuwa na ziara ya Marekani.

Alisema kwamba tuhuma hizo zinazomkabili Diddy zinakaa kisheria Zaidi na hivyo asingeweza kuzizungumzia hadi pale wachunguzi wakamilishe uchunguzi wao.

“Kwanza kabisa nisingependa kujifanya mchambuzi sana kwenye tukio lake kwa sababu sijazomea sheria. Kwa hiyo kwa ukweli ni mpaka mahakama au mamlaka zao zitakaposema hapo... lakini siwezi sema nimhukumu au nimkatalie hapana.”

“Lakini nashukuru Mungu katika moja ya ziara zangu za Marekani tulienda mimi na Babu Tale na Swizz Beatz, alitualika kwake tukapata chakula pale nini, unajua kulikuwa na familia yake, watoto na wasanii wake wapya kwa hiyo, alinishauri kidogo kwenye muziki, licha ya kwamba kuna vitu vyovyote wao watakavyozungumza lakini mimi nilimheshimu kama msanii, na mtu ambaye katika muziki anajua vitu vingi sana,” Diamond alimkingia kifua P Diddy.

P Diddy amekuwa chini ya uchunguzi kwa wiki kadhaa sasa baada ya watu mbalimbali kujitokeza na kudai kwamba amewahi wadhulumu kingono.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved