logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Watu 6 kuhukumiwa kwa mauaji ya mbunge wa zamani, George Thuo

Sita hao walishirikiana katika kumtilia sumu mbunge huyo kwenye klabu ya Porkies katika kaunti ya Kiambu

image
na

Habari21 June 2024 - 07:51

Muhtasari


•Sita hao walishirikiana katika kumtilia sumu mbunge huyo kwenye klabu ya Porkies katika kaunti ya Kiambu.

•Mke wa hayati Thuo aliiambia korti kuwa mumewe alikuwa mwenye buheri wa afya kabla ya kupatana na washukiwa hao siku hiyo ya maafa

Watu sita waliopatikana na hatia ya mauaji ya aliyekuwa mbunge wa zamani wa Juja George Thuo watarajiwa kuhukumiwa hii leo.

Mahakama kuu ya Milimani mnamo Aprili mwaka huu iliagiza kuwa sita hao walishirikiana katika kumtilia sumu mbunge huyo kwenye klabu ya Porkies katika kaunti ya Kiambu.

Kisa hiki kilitukia mnamo mwaka 2013 ambapo mbunge huyo alitiliwa sumu ya wadudu aina ya cyhalothrine.

Sita hao ni: Esther Mulinge, Samuel Kuria Ngugi, Christopher Lumbazio, Ruth Watahi Irungu,Andrew Karanja Wainaina na Paul Wainaina Boiyo.

Wakati wa maendeleo ya kesi hii mnamo Mei 28, waendeshaji mashtaki walirai korti iwahukumu washukiwa adhabu ya juu zaidi. 

Vilevile, waendeshaji hao walisisitiza kuwa washukiwa hao wasionyeshwe huruma kwani hawakuwa na majuto wakati wakishiriki uhayawani huu.

Mke wa hayati Thuo aliiambia korti kuwa mumewe alikuwa mwenye buheri wa afya kabla ya kupatana na washukiwa hao siku hiyo ya maafa.

“Alipopatiwa fursa ya kuzungumza, mkewe Thuo alimwambia hakimu Roseline Korir kuwa mumewe alikuwa na siha njema kabala ya kifo chake cha ghafla, ambacho kilifanyika akiwa pamoja na washukiwa hawa,” Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP) ilisema kwenye mashtaka.

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved