logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanamke ameza sindano ya kushona - Kirinyaga

Ipo haja ya hali ya matibabu kuboreshwa kwa wasiojiweza

image
na

Habari15 August 2024 - 05:52

Muhtasari


•"Tuna hofu yakua huenda tukampoteza.

• Naomba msaada ili mke wangu apate matibabu

EVERLINE KAREKIA

Mwanamke mwenye umri wa miaka 31 kwa jina la Erveline Kareika kutoka  kijiji cha Mugambaciura kaunti ya Kirinyaga, ameshangaza wengi kwa kudai kumeza sindano ya kushona nguo.

Everline alisema anapitia kipindi kigumu na kwamba bado hajapata matibabu yoyote na kuomba msaada kutoka kwa wasamaria wema kufadhili matibabu yake.

 Mumewe Kelvin Maina ,kwa mahojiano na wanahabari ,alisema kuwa kisa hiki kilitendeka wakati alipokua akimlisha mwanawe wa miezi minane, alipomaliza kushona na kueka sindano kwenye kinywa chake na kisha kuumeza kwa ghafla.

Aidha ,Maina asema hatua yake ya kumpeleleka mkewe hosipitalini huko Embu haikuzaa matunda   licha ya kulipa sh.800 ili kufanyiwa x-ray.

Vilevile bwana Maina anasema haikua safari ya mwisho na kwamba walichukua hatua ya kwenda Kerugoya ambapo walitozwa sh.10,000 ambazo hakua nazo nakulazimika kuridi nyumbani huku sindano ikiwa imekwama kwa koo ya bibiye.

"Tuna hofu kuwa huenda tukampoteza na kwa hivyo  ndiposa naja kwenu kuomba msaada ili apate matibabu zaidi" Maina alisema kwa huzuni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved