logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mfichuzi wa sakata ya Adani adai anatafutwa na maafisa wa polisi

Nelson Amenya amesema maafisa wa DCI walifika nyumbani kwa wazazi wake na kwa karakana ya rafiki wakidai kutafuta gari lililoibwa

image
na Brandon Asiema

Habari30 October 2024 - 09:56

Muhtasari


  • Nelson ameitaka idara ya DCI kutumia rasilimali za thamani ilizonazo kupigana na mauaji ya wanawake yaliyokithiri na uhalifu pamoja na ufisadi katika sekta za umma.
  • Amenya amewatahadhari maafisa hao kuwa anawajua na ikiwa kitu chochote kitawafanyikia watu walio karibu naye dunia nzima itafahamu majina yao.


Mkenya aliyefichua mpango wa serikali kukodisha uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta Nelson Amenya sasa anadai kuwa maafisa wa polisi wa kitengo cha upelelezi DCI wanamtafuta.

Amenya amesema kuwa maafisa hao aliowataja kama Subaru Gang, walifikia nyumabni kwao na kwa karakana ya rafiki wake siku chache zilizopita kwa madai ya kutafuta gari lililodaiwa kuibwa.

Kwa mujibu wa Amenya, maafisa hao wa polisi walifika nyumbani kwa wazazi wake wakidai kuwa walipata taarifa ya gari lililoibiwa kuwa limeegeshwa katika boma lao. Aliongeza kusema kuwa polisi hao walifanya msako hadi kwa paa ya ghorofa kisha wakaondoka.

Baada ya kuondoka nyumbani kwa wazazi wake, Amenya amesema kuwa mafisa hao walienda kwa karakana ya rafiki yake ambapo walidai kuwa walikuwa wanatafuta gari aina ya Mercedes muundo wa kisasa lililokisiwa kuwa sehemu hiyo.

“Baadaye, walienda kwa karakana ya rafiki mara hiyo wakisema walikuwa wanatafuta gari aina ya Mercedes muundo mpya lililoibwa wa walikuwa na habari lilikuwa pale.” Aliandika Amenya kwenye ukurasa wa X.

Aidha, Amenya amewatahadharisha maafisa hao kuwa anawajua na ikiwa kitu chochote kitawafanyikia watu walio karibu naye dunia nzima itafahamu majina yao.

Hata hivyo, amekashifu idara ya DCI kwa madai ya kutumia rasilimali za thamani kumlenga mkenya asiye na madhara kwa sababu ya kufichua siri ya mkataba baina ya Adani na JKIA.

Ameitaka idara hiyo badala yake kutumia rasilimali hizo kupigana na mauaji ya wanawake yaliyokithiri na uhalifu pamoja na ufisadi katika sekta za umma

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved