logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Wengine wananiambia wako na inches!" Esther Passaris alalamika kuhusu kutumiwa picha za uchi na vijana, awaomba kukoma

Passaris alitaja kitendo hicho kuwa ni ukosefu wa heshima na kuwataka wakome.

image
na Samuel Mainajournalist

Habari30 October 2024 - 07:11

Muhtasari


  • "Mimi niko na miaka sitini, alafu unaniambie uko na inches, alafu unatoa suruali, unachukua picha, ata haijasimama, unanitumia. Unaniambie nifanye nini nayo?," Passaris alihoji.
  • Passaris aliwataka vijana hao kuwa na heshima huku akiwaonya kuwa Mungu aliye mbinguni anatazama matendo yao.

Mwakilishi wa kike wa kaunti ya Nairobi Esther Muthoni Passaris ameibua wasiwasi kuhusu unyanyasaji wa mtandaoni na wa kijinsia na baadhi ya vijana wa Kenya.

Wakati akizungumza katika hafla ya hivi majuzi, mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 60 alifichua kuwa baadhi ya vijana wamekuwa wakimtumia picha za sehemu za siri tangu nambari yake ilipovujishwa kwenye mitandao ya kijamii mapema mwaka huu.

Passaris alitaja kitendo hicho kuwa ni ukosefu wa heshima na kuwataka wakome huku akieleza kwamba amehitimu kuwa mama kwa wale wanaomtumia picha hizo za utupu.

“Vijana, tafadhali. Sijui ni nini imetendeka na vijana wetu. Na tutakuwa na mpango wa kuwawezesha vijana ili tuzungumze vizuri. Kwa sababu, mimi nimeona ata mimi kama mheshimiwa, saa wengine vijana wananikosea heshima,” Esther Passaris alilalamika.

Aliendelea,“Unajua ile wakati niliweka namba yangu kwenye mtandao, wakaanza kusalimia kila mtu, wamenitumia mapicha ya vitu ambavyo ata sijui wanafikiria nini hiyo kitu, lazima niiangalie. Wengine wananiambia wako na ma-inches, sasa mimi najiuliza kama Watoto wangu, Mimi niko na miaka sitini, alafu unaniambie uko na inches, alafu unatoa suruali, unachukua picha, ata haijasimama, unanitumia. Unaniambie nifanye nini na hiyo kitu? Sasa unataka nifanyeje? au hata labda sio yako, umechukua picha kwa mtandao, kwa sababu hiyo huwezi piga picha, kwa sababu ukipiga picha haionekani.”

Mwanasiasa huyo ambaye alipigiwa kura kwa tikiti ya chama cha ODM aliwataka vijana hao kuwa na heshima huku akiwaonya kuwa Mungu aliye mbinguni anatazama matendo yao.

Nambari ya simu ya Passaris ni miongoni mwa nambari ambazo zilivunjishwa kwenye mitandao ya kijamii wakati wa maandamano ya vijana nchini kote miezi michache iliyopita.

Vijana kwenye mitandao ya kijamii walivujisha namba za wanasiasa mbalimbali ambao walikuwa na hasira nao na kuwataka wenzao ‘kuwasalimia’.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved