Rais William Ruto amejumuika na viongozi wengine katika kufariji familia ya aliyekuwa Seneta wa Embu, Lenny Kivuti, kufuatia kifo cha mwanawe, Eric Mutugi.
Katika taarifa yale iliyotolewa Jumatatu Disemba 23, rais Ruto alisema kuwa nyota ya Mutugi imezima mapema huku ahadi alizokuwa nazo zikikzimwa.
Kiongozi huyo wa taifa aliendelea kusema kuwa anaiombea familia ya Kivuti wakati huu wa kipindi kigumu cha maombolezo wanapokabiliana na msiba wa mtoto wao.
Vile vile kwenye ujumbe wake kupitia anwani ya X, rais pia aliomba faraja ya Mungu kwa familia na marafiki wa Kivuti.
“Naungana na familia ya Mheshimiwa Lenny Kivuti katika maombolezo ya msiba wa mwanawe mpendwa, Eric Mutugi. Ninaiombea familia ya Kivuti katika kipindi hiki kigumu sana. Nuru na ahadi ya Eric imechukuliwa hivi karibuni, Mungu awape familia na marafiki nguvu, faraja na amani,” Ruto alisema.
Lenny Kivuti alihudumu kama Seneta wa kwanza wa kaunti ya Embu kuanzia 2013 hadi 2017. Kabla ya kuwa
seneta Kivuti awali alihudumu kama mbunge wa Siakago.
Seneta huyo wa zamani alifichua kuwa mwanawe
aliaga dunia katika hospitali ya MP Shah baada ya kuugua kwa muda mfupi.
