logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshukiwa wa ulanguzi wa dawa za kulevya akamatwa na kuzuiliwa

Mshukiwa huyo alikuwa amepanga misokoto ya bangi kkwenye buti ya gari lake

image
na Brandon Asiema

Habari09 January 2025 - 07:56

Muhtasari


  • Polisi wanamsaka mshukiwa wa pili aliyetoroka wakati wa msako wa polisi katika eneola Kiembeni.
  • Gunia sita za bangi zilipatikana katika nyumba moja karibi na shule ya Kiembeni.


Polisi wa kupambana na ulanguzi wa dawa za kulevywa katika kaunti ya Mombasa wanamzuilikwa mshukiwa mmoja anayedaiwa kuhusika katika ulanguzi wa mihadarati.

Mshukiwa huyo amabye alikamatwa katuika barabara kuu ya Nairobi – Mombasa mnamo Jumatano, alikuwa akiendesha gari aina ya Toyota Axio katika eneo la Jomvu.

Msako wa polisi kwenye gari lake ulibaini upatikanaji wa misokoto ya bangi iliyokuwa imefichwa kwenye buti ya gari hiyo. Kwa mujibu wa idara ya upelelezi kwenye ujumbe wake kwa anwani yake ya X, imesema kuwa walanguzi wa mihadarati wanajaribu kutumia mbinu mbali mbali ya kusafirisha dawa za kulevya.

Katika kisa kingine kwenye kaunti hiyo ya Mombasa, mshukiwa mwingine alifanikiwa kutoroka baada ya maafisa wa usalama kufanya msako dhidi ya mihadarati katika maeneo ya karibu na shule ya msingi ya Kiembeni.

Kwenye msako huo, maafisa wa polisi kutoka kituo cha Kiembeni walifanikiwa kupata gunia sita za bangi.Hata hivyo msako wa kumtafuta mshukiwa huyo unaendeshwa.

Hata hivyo mshukiwa wa kwanza aliyekamatwa katika eneo la Jomvu, abnnazuiliwa na polisi katika kituo cha polisi cha Jomvu pamoja na mihadarati aliyopatikana nayo ambapo atafikishwa mahakamani baadaye kujibu mashtaka atayoshtakiwa nayo.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved