logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Matiang’i Ni ‘Tax Collector’ Mkubwa Hata Kuliko Ruto, Hawezi Kuwa Rais! – Francis Atwoli

“Kila Mkenya anajua vizuri sana kwamba kama siasa za Kenya zilikuwa zinaamuliwa kwa masuala tata, basi leo hii Atwoli angekuwa rais wa Jamhuri ya Kenya,” Atwoli alisema.

image
na MOSES SAGWEjournalist

Habari29 January 2025 - 12:05

Muhtasari


  • Alidai kwamba waziri huyo wa zamani hakuwahi mpigia kampeni hata siku moja mgombea wa upinzani Raila Odinga kuelekea uchaguzi wa 2022.
  • “Wakati tulikuwa katika Azimio na tulikuwa tunatoka, Matinag’i hakuwahi hata mpigia kampeni Raila. Hakuonekana mahali popote akimpigia debe Raila." 



KATIBU mkuu wa muungano wa wafanyikazi nchini COTU, Francis Atwoli ameibua cheche za kisiasa baada ya kuwazomea baadhi ya wanasiasa wanaojikusanya tayari kumtoa rais Ruto ofisini katika uchaguzi wa 2027.


Akizungumza Januari 28 na waandishi wa habari, Atwoli alisema kwamba wanasiasa wote ambao wanahaha juu na chini kwa lengo la kumshinda Ruto wanafanya kazi bure, akisema kuwa siasa za Kenya hazishindwi kuzungumzia mahitaji ya wakenya bali kwa kujikusanyia watu kimaeneo.


Atwoli alisema kwamba hata Fred Matiang’i – waziri wa zamani wa usalama wa ndani ambaye anapigiwa debe na baadhi ya Wakenya hawezi kuwa rais, akimtaja kuwa mtoza ushuru mbaya zaidi hata kuliko rais Ruto mwenyewe.


“Mnataka kuniambia Matinag’i anaweza kuwa rais wa jamhuri ya Kenya? Mimi mwenyewe nimefanya kazi na Matiang’i. Yeye ni mtoza ushuru, zaidi ya William Ruto. Mimi namjua,” Atwoli alisema.


Alidai kwamba waziri huyo wa zamani hakuwahi mpigia kampeni hata siku moja mgombea wa upinzani Raila Odinga kuelekea uchaguzi wa 2022 licha ya kuwa bosi wake Uhuru Kenyatta ndiye alikuwa anaongoza kampeni za Odinga.


“Wakati tulikuwa katika Azimio na tulikuwa tunatoka, Matinag’i hakuwahi hata mpigia kampeni Raila. Hakuonekana mahali popote akimpigia debe Raila. Walikuwa bize katika ofisi ya rais wakitengeneza pesa. Mimi namjua kwa sababu nilikuwepo,” Atwoli alisisitiza.


Atwoli alisema kwamba hakuna Mkenya ambaye amepigania haki za Wakenya zaidi kumliko na kueleza kwamba ingekuwa kura zingepigwa kwa msingi huo basi yeye angekuwa rais.


“Kila Mkenya anajua vizuri sana kwamba kama siasa za Kenya zilikuwa zinaamuliwa kwa masuala tata, basi leo hii Atwoli angekuwa rais wa Jamhuri ya Kenya,” Atwoli alisema.


“Lakini ukweli ni kwamba siasa za Kenya zimejikita katika ukabila,” aliongeza.


Mzee Atwoli alipuuzilia mbali uwezekano wa muungano mkubwa zaidi kuundwa ili kumtoa Ruto mamlakani 2027 akisema kwamba Azimio ndio ulikuwa muungano mkubwa kabisa lakini bado hawakufanikiwa kushinda urais.


“Nilikuwa ndani ya Azimio, tulikuwa na muungano mkubwa zaidi kuliko ule ambao wanataka kuanzisha sasa lakini tukashindwa,” alifoka.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved