logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mama ataka kuuza Figo kuwasaidia wanawe ambao ni waraibu

Mama alizungumza kwa uchungu akisisitiza kwamba yuko tayari kuyapoteza maisha yake ila watoto wake wasaidiwe.

image
na Japheth Nyongesa

Habari26 March 2025 - 14:46

Muhtasari


  • Philomena Alimo mwenye umuri wa miaka 45, ameeleza kwamba ndoa yake ilisambaratika miaka 13.
  • Na watoto wake ndio walikua wamebaki kama matumaini ila pia wameamua kuingilia mihadharati.
Kidney
Mwanamke mmoja kutoka katika kaunti ya Nandi amewashangaza wengi baada ya kuandika kwenye kibao akitafuta soko ya kuuza figo zake zote ili kuwatafutia matibabu watoto wake wawili.

Mama huyo amefichua kwamba amefikia maamuzi hayo baada watoto wake hao ambao ni wa kiume kuendelea kudhofika kiafya baada ya kuathirika kutokana na matumizi ya dawa za kulevya.

Philomena Alimo mwenye umuri wa miaka 45, ameeleza kwamba ndoa yake ilisambaratika miaka 13, na watoto wake ndio walikua wamebaki kama matumaini ila pia wameamua kuingilia mihadharati.

"Mimi kama mama ya watoto hao wawili, nilipoona hao vijana wakiwa wameharibika hivyo na maisha yao ya hapo mbeleni hakuna matumaini. Nimeamua kuuza figo zangu mbili, moja ya mtoto wangu wa kwanza na nyingine ya mtoto wangu wa pili," alieleza mwanamke huyo.

Nimeishi maisha yangu na sioni haja ya kuishi wakati watoto wangu wwanaangamia. Ndiposa nimechukua hii hatua na nimeamua kuuza  figo zote mbili,' aliendelea.

Mama huyo wa watoto wawili ameeleza kwamba aliamua kuchukua maamuzi hayo baada ya juhudi zake za kutafuta usaidi kutoka kwa watu tofauti tofauti na ofisi mbalimbali kugonga mwamba.

"Kabla hata sijachukua hii hatua, nimezunguka kwote nikitafuta msaada ili vijana wangu hao wawili waweze kusaidiwa na wapelekwe katika madaktari wa kuwasaidia,' alisema.

Nimeenda kwa maaskofu, wachungaji, serikali, nimeenda kwa advocates ili kuuliza namna ya kuweza kusaidia hawa vijana. Nimetembelea jamii, nimeuliza marafiki lakini sijaweza kupata msaada,' aliweka wazi Alimo.

Mama huyo ambaye alizungumza kwa uchungu amesisitiza kwamba yuko tayari kuyapoteza maisha yake ila watoto wake wasaidiwe kurejelea hali yao ya awali.

'Najua ni maamuzi magumu ambaye nimechukua, lakini sioni ubaya kupoteza maisha yangu kwa ajili ya watoto wangu," Mwanamke huyo alisimulia kwa uchungu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved