logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kindiki Aapa Kukomesha "Madharau Na Kiburi" Ya Gachagua Nchini

Kindiki alimshambulia Gachagua akisema atakomesha sarakasi zake kwa namna ya kipekee na isiyo na mjadala.

image
na Tony Mballa

Habari23 June 2025 - 08:36

Muhtasari


  • Kwa sasa, Kindiki anaendesha ziara za kuwawezesha wananchi katika eneo hilo akiwa ameandamana na wabunge waliochaguliwa, ambao Gachagua amewataja kuwa wasaliti wa eneo la Mlima Kenya na ambao anasema wanapaswa kuondolewa afisini katika uchaguzi wa 2027.
  • Lengo la Gachagua kulinda eneo la Mlima Kenya linawakilisha changamoto kubwa ya kisiasa kwa Kindiki, ambaye atakabiliwa na kibarua kigumu cha kuleta kura za maana kwa Ruto endapo watawania urais kwa pamoja.

Naibu Rais Kithure Kindiki ameapa kukabiliana na Kiongozi wa Chama cha Democracy for Citizens (DCP) Rigathi Gachagua, wakati mvutano kuhusu udhibiti wa ngome yenye kura nyingi ya eneo la Mlima Kenya ukizidi kupamba moto.

Katika taarifa kali siku ya Jumapili, Juni 22, 2025, Kindiki alimshambulia Gachagua akisema atakomesha sarakasi zake kwa namna ya kipekee na isiyo na mjadala.

“Bwana Trap Man, maisha yako mafupi na yaliyojaa kashfa kisiasa yamekuwa yakiendelea kupitia vitisho vya juujuu, majivuno, kiburi na kutojali,” Kindiki alisema.

“Kwa kuwa nia yako ni kutuvuruga, sisi tutaendelea kuzingatia jukumu muhimu la kuijenga Kenya kama tunavyotakiwa na wajibu wa ofisi.”

Kithure Kindiki

“Hata hivyo, bado tutapata muda wa kukukabili moja kwa moja na kuangamiza sarakasi zako za kipuuzi na utoto kwa njia ya kipekee na isiyo na shaka. Umekosea kwa ujinga,” Kindiki aliongeza.

Kauli hiyo ilijiri siku moja baada ya Kindiki kutoa taarifa nyingine ambapo alimkosoa Gachagua kwa kuunda misemo inayolenga kuongeza umaarufu wake wa kisiasa nchini.

“Wale ambao ujumbe wao pekee ni nderemo kuhusu nani atakuwa ofisini kwa muda gani au nani anazungumza kwa sauti gani, watasombwa na mafuriko ya umma unaozidi kuwa werevu, umefumbuka macho na usio na mchezo – umma usioweza tena kununua upumbavu kutoka kwa wapumbavu wa kisiasa, bandia, matapeli na mizigo,” ilisoma taarifa hiyo.

“Haya madharau na kiburi yataisha; ni suala la muda tu,” aliongeza.

Kithure Kindiki

Katika mapambano ya kuwania udhibiti wa eneo la Mlima Kenya, viongozi hao wawili wamejitosa vilivyo kuwania mioyo na nafsi za watu, kila upande ukiahidi maisha bora ya baadaye.

Ingawa Kindiki anasalia kuwa mwanasiasa wa juu zaidi wa eneo hilo kwa nafasi yake ndani ya serikali ya Kenya Kwanza, mashambulizi ya Gachagua katika eneo hilo yamevutia baadhi ya wanasiasa wakuu upande wake, hali inayotishia ushawishi wa Kindiki huku zikiwa zimesalia chini ya miaka miwili kabla ya uchaguzi mkuu.

Kwa sasa, Kindiki anaendesha ziara za kuwawezesha wananchi katika eneo hilo akiwa ameandamana na wabunge waliochaguliwa, ambao Gachagua amewataja kuwa wasaliti wa eneo la Mlima Kenya na ambao anasema wanapaswa kuondolewa afisini katika uchaguzi wa 2027.

Lengo la Gachagua kulinda eneo la Mlima Kenya linawakilisha changamoto kubwa ya kisiasa kwa Kindiki, ambaye atakabiliwa na kibarua kigumu cha kuleta kura za maana kwa Ruto endapo watawania urais kwa pamoja.

Kithure Kindiki

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved