logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Murkomen: Polisi Watakabiliana Vikali na Wahalifu Siku ya Saba Saba

Aliahidi kuhakikisha kuwa watu wanaosababisha fujo wakati wa maandamano wanachukuliwa hatua za kisheria.

image
na Tony Mballa

Habari07 July 2025 - 11:58

Muhtasari


  • Akizungumza Jumapili wakati wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya Kanisa Katoliki katika eneobunge la Tigania Magharibi, kaunti ya Meru, Murkomen alitangaza kuwa Tigania Magharibi itagawanywa na kuwa kaunti ndogo mbili zaidi.
  • Akizungumzia suala la usalama katika mpaka wa Tigania, Igembe na Isiolo, waziri huyo alisema kuwa wizara yake inafanya kazi kwa bidii kutokomeza ukosefu wa usalama na uhalifu wa kutumia silaha katika maeneo hayo ya mpakani.

Waziri wa Usalama wa Ndani Kipchumba Murkomen amewahimiza Wakenya kudumisha amani kabla ya maandamano yaliyopangwa ya Saba Saba.

Murkomen alisema kuwa maafisa wa polisi hawapaswi kulaumiwa kwa kushughulikia hali zinazotishia usalama wa umma wakati wa maandamano.

Aliahidi kuhakikisha kuwa watu wanaosababisha fujo wakati wa maandamano wanachukuliwa hatua za kisheria.

Waziri huyo aliwataka polisi waendelee kuwa na urafiki kwa wananchi, lakini wachukue hatua kali dhidi ya wahuni wanaotumia maandamano kama kisingizio cha kuharibu mali.

“Polisi wanapaswa kuchukua hatua dhidi ya wahuni na waandamanaji wanaonuia kusababisha vurugu wakati wa maandamano,” alisema.

Akizungumza Jumapili wakati wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya Kanisa Katoliki katika eneobunge la Tigania Magharibi, kaunti ya Meru, Murkomen alitangaza kuwa Tigania Magharibi itagawanywa na kuwa kaunti ndogo mbili zaidi.

Akizungumzia suala la usalama katika mpaka wa Tigania, Igembe na Isiolo, waziri huyo alisema kuwa wizara yake inafanya kazi kwa bidii kutokomeza ukosefu wa usalama na uhalifu wa kutumia silaha katika maeneo hayo ya mpakani.

Aliwapongeza maafisa wa polisi kwa kazi yao nzuri na kujitolea kwao kulihudumia taifa.

Murkomen pia aliwahimiza wafugaji kushirikiana kwa karibu na polisi ili kukomesha wizi wa mifugo.

Mbunge wa Tigania Magharibi John Mutunga alidai kuwa viongozi wa upinzani ni wapiga kelele tu wasiokuwa na ajenda yoyote ya maana kwa taifa.

Aliwataka wakazi wa Meru kumuunga mkono rais kwa ajili ya maendeleo ya eneo hilo.

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved