logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Arsenal Kupimana Ubabe na West Ham Ugani Emirates Jumamosi

Dabi ya London yajaa msisimko: Arsenal wakabiliana na West Ham Emirates

image
na Tony Mballa

Habari03 October 2025 - 19:42

Muhtasari


  • West Ham chini ya Nuno Espirito Santo wanatafuta ushindi wa kihistoria Emirates, huku Arsenal ikitafuta ushindi wa nne mfululizo katika mashindano yote.
  • Mchezo huu unatarajiwa kuwa na mvutano mkubwa.

LONDON, UINGEREZA, Ijumaa, Oktoba 3, 2025 – Klabu ya Arsenal inatarajiwa kushuka dimbani Emirates Stadium Jumamosi saa kumi alasiri kwa mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya West Ham United.

Makocha Mikel Arteta na Nuno Espirito Santo wanakutana kwa mara ya kwanza katika dabi hii ya London yenye ushindani mkubwa.

Arsenal imekuwa na changamoto dhidi ya West Ham katika michezo ya nyumbani. Katika mechi nne za mwisho Emirates, Gunners wamepoteza mara mbili kwa Hammers.

Ikiwa West Ham watashinda tena, watakuwa timu ya pili pekee katika historia ya ligi kushinda mara tatu mfululizo ugenini dhidi ya Arsenal.

Kauli za makocha

Mkufunzi mkuu wa Arsenal Mikel Arteta/ARSENAL FACEBOOK 

Kocha wa Arsenal amesema anataka timu yake kuvunja nuksi ya kupoteza mara mbili mfululizo dhidi ya West Ham nyumbani.

“Tunataka kuendelea kucheza kwa kasi na kushinda mechi muhimu. Tunajua West Ham ni wapinzani wagumu na tunahitaji kujibu changamoto hii,” amesema Arteta.

Ameongeza kuwa mashabiki wanatarajia matokeo chanya: “Tunajua wanataka ushindi, na jukumu letu ni kuhakikisha tunawapa sababu ya kufurahia.”

Nuno Espirito Santo

Kocha wa klabu ya West Ham Nuno Espirito Santo/WEST HAM FACEBOOK 

Kocha mpya wa West Ham amesema anataka kikosi chake kuonyesha mshikamano. “Kila mtu ndani ya klabu amejitolea.

Tunapaswa kucheza kwa ujasiri na nidhamu. Tunahitaji kuwa imara na kushindana katika kila dakika,” amesema Nuno.

Ameongeza kuwa mashabiki ni nguvu ya timu: “Tunapotembea na mashabiki nyuma yetu, wachezaji wanajisikia huru. Tunataka kuwarudishia furaha kupitia matokeo.”

Habari za majeruhi

Arsenal huenda wakakosa beki Gabriel ambaye alitolewa uwanjani dhidi ya Olympiacos. Hincapie bado anauguza jeraha la groin, huku Havertz, Jesus na Madueke wakiwa nje. Kwa West Ham, Tomas Soucek atakosa mechi kwa sababu ya kadi nyekundu, na chipukizi George Earthy ameumia paja.

PICHA YA JALADA: Wachezaji wa Arsenal washerehekea bao lao/ARSENAL FACEBOOK 

Makala Zinazohusiana


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved