logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Inauma! Mwili wa 2Pac wa Ghana wasimamishwa kando ya jeneza kupewa heshima ya mwisho (+picha)

Alizikwa kwenye jeneza la rangi ya dhahabu lililokuwa na lebo ya Tiktok.

image
na Radio Jambo

Football04 May 2023 - 08:51

Muhtasari


•Mamia ya waombolezaji wakiwemo wanafamilia, marafiki, wasanii na watu wengine mashuhuri walihudhuria hafla hiyo iliyojaa hisia.

•Kabla ya kuzikwa, mwili wa Ahoufe ulitolewa nje ya jeneza ili kuwaruhusu waombolezaji kumpa heshima za mwisho.

2pac Shakur wa Ghana,  Ahoufe Abrantie hatimaye alizikwa mwishoni mwa mwezi jana.

Mtumbuizaji huyo wa Tiktok mwenye maumbile ya kipekee ambaye alijizolea umaarufu mkubwa kote duniani kupitia video zake za kusisimua alizikwa nyumbani kwao katika eneo la Kumasi, Ghana mnamo Aprili 29.

Mamia ya waombolezaji wakiwemo wanafamilia, marafiki, wasanii na watu wengine mashuhuri walihudhuria hafla hiyo iliyojaa hisia. Alizikwa kwenye jeneza la rangi ya dhahabu lililokuwa na lebo ya Tiktok.

Kabla ya kuzikwa, mwili wa Ahoufe ulitolewa nje ya jeneza ili kuwaruhusu waombolezaji kumpa heshima za mwisho.

Video za mazishi hayo ambazo zilifikia Radio Jambo ziliwaonyesha waombolezaji wakifanya matambiko mbalimbali kwenye mwili wa mtumbuizaji huyo huku wengine wao wakiangua kilio kikubwa baada ya kuutazama mwili. Mwili wa marehemu Ahoufe uliokuwa umevalishwa shati ya bluu, bandana kichwani na mnyororo shingoni ulitulia pembeni ya jeneza huku waombolezaji wakitoa heshima za mwisho.

Staa huyo wa TikTok aliaga dunia mnamo Machi 30 katika nyumba yake jijini Kumasi, Ghana. Kifo cha Ahuofe ambaye alijulikana sana kwa kuvaa na kuzungumza kama ‘jambazi’ kiliwashangaza wengi ambao walimuomboleza kwa hisia.

Video zake zilihusu kuiga haiba ya marehemu rapa wa Marekani, Tupac Amaru Shakur.

Huku akimuomboleza, mama yake alisema, "Alilazwa hospitalini kwa siku mbili kabla ya kifo chake. Uvumi kwamba alikuwa akitumia dawa za kulevya ni uongo. Nilitokwa na machozi daktari alipothibitisha kifo chake. Nawashukuru mashabiki wake kwa upendo. Mungu atusaidie."

Mamake Ahuofe ambaye anajulikana sana kama Mama gee alisema ilimletea furaha kuona jinsi mwanawe alivyosababisha furaha kubwa kwenye mitandao ya kijamii.

"Hakuwa na tatizo la kiafya," alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved