logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa akamatwa kwa madai ya kumuua mkewe na kuchoma mwili wake

Polisi walikuta mwili wa marehemu ukiwa bado unawaka moto na umechomeka kabisa.

image
na Radio Jambo

Habari25 August 2022 - 12:01

Muhtasari


•Titus Nderitu  anadaiwa kumuua mpenziwe nyumbani kwao kabla ya kutumia gari lake kusafirisha maiti hadi kijiji cha Pesi alikochomea mwili.

•Awali polisi walikuwa wakichukulia kisa hicho kama kisa cha utekaji nyara.

Polisi huko Nyandarua wanamzuilia mwanamume mmoja kwa tuhuma za kumuua mpenziwe kikatili,na kuchoma mwili wake.

Kulingana na ripoti ya polisi, Titus Nderitu Gichohi, anadaiwa kumuua mpenziwe nyumbani kwao kabla ya kutumia gari lake kusafirisha maiti hadi kijiji cha Pesi, eneo bunge la Ndaragua, ambapo inadaiwa aliiuchoma moto ili kuharibu ushahidi wowote ambao ungemhusisha na mauaji.

''Uchunguzi wa matukio hayo unaonyesha kuwa mwathiriwa aliuawa ndani ya nyumba yake na mwili wake kuhamishwa hadi eneo la nyingine ambapo mshukiwa aliuchoma katika juhudi za kuharibu ushahidi,” Ripoti ya polisi imesema.

Awali polisi walikuwa wakichukulia kisa hicho kama kisa cha utekaji nyara kabla ya wakaazi wa eneo hilo kutoa taarifa kwamba walikuwa wameona gari la marehemu nyumbani kwa Gichohi.

Hili liliwafanya wapelelezi kuzuru eneo la tukio, ambapo walikuta mwili wa marehemu ukiwa bado unawaka moto na kuchomeka kabisa.

Kulingana na Naibu Kamishna wa Kaunti Ndogo ya Aberdare Charles Rukwaro, mshukiwa hakuwa katika eneo la tukio wakati huo lakini inasemekana alikamatwa na polisi eneo la Kasarani alipokuwa akijaribu kutoroka.

Mwili wa marehemu umehamishiwa katika hospitali ya Nyahururu kaunti ya Laikipia.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved