logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jambo maalum analofanya mwajiri wa Rosie kuhakikisha anawatendea watoto wao vyema

Waajiri wa Rosie wameendelea kushiriki video za muungano wake mzuri na familia yao na kuelezea furaha yao juu yake.

image
na Radio Jambo

Habari24 January 2024 - 08:07

Muhtasari


•Waajiri wa Rosie wameendelea kushiriki video za muungano wake mzuri na familia yao na kuelezea furaha yao juu yake.

•Alifichua kuwa kurejea kwa Rosie kutamwezesha kusafiri duniani kwani ana uhakika watoto wake watakuwa katika mikono salama.

amerejea Lebanon kwa mwajiri wake.

Mwajiri wa mwanamke wa Kenya aliyevuma Roseline Atieno almaarufu Nanny Rosie ameendelea kusherehekea kurejea kwake nchini Lebanon.

Rosie ambaye amekuwa akiwafanyia kazi wanandoa maarufu wa Lebanon tangu 2021 alikuwa amerudi Kenya mwishoni mwa mwaka jana na alirejea katika nchi hiyo ya Mashariki ya Kati mapema wiki hii, takriban miezi miwili baadaye.

Kufuatia kurejea kwake, waajiri wa Rosie wameendelea kushiriki video za muungano wake mzuri na familia yao na kuelezea furaha yao juu yake.

"Rosie alitimiza ahadi yake na kurudi kwa mapacha ingawa alipata ofa nyingi. Upendo wa kweli utashinda kila wakati," waajiri wa Rosie walisema kupitia mitandao ya kijamii.

Katika video nyingine inayomuonyesha Rosie akiwa amebeba mapacha hao ambao amekuwa akisaidia kulea, mwajiri huyo alidokeza kuhusu sababu maalum inayomfanya mwanamke huyo anayetoka eneo la Bondo, kaunti ya Siaya kuwatendea vyema watoto wake.

"Mtendee kama malkia, atawachukulia watoto wako kama wake. Asante Rosie,” mwajiri alisema.

Pia alifichua kuwa kurejea kwa Rosie sasa kutamwezesha kuendelea kusafiri duniani kwani ana uhakika watoto wake watakuwa katika mikono salama.

“Sasa ninaweza kusafiri kwa amani baada ya Rosie kurudi. Instabul nakuja," alisema.

Rosie ambaye alipata umaarufu mwishoni mwa mwaka jana kufuatia video yenye hisia kali ya yeye akiiga familia ya mwajiri wake alirejea Lebanon Jumatatu baada ya kuwa na familia yake nchini Kenya kwa karibu miezi miwili. Waajiri wake na watoto wao wawili walimkaribisha kwenye uwanja wa ndege ambapo walikuwa na muungano mzuri sana.

Katika mahojiano ya Desemba mwaka jana baada ya kurejea Kenya, Rosie alisema alijisikia vibaya sana kuwaacha wanandoa ambao amewafanyia kazi tangu Oktoba 2021 pamoja na watoto wao wanne ambao alikuwa akiwatunza.

"Ilikuwa wakati wa huzuni zaidi maishani mwangu. Ilijawa na hisia tofauti kwa sababu kwa upande mmoja nilifurahi kuja kukutana na familia yangu na kwa upande mwingine nilikuwa na huzuni kwa sababu nilikuwa naacha watoto ambao nimeishi nao kwa miaka miwili,” Rozzie alisema.

Mwanamke huyo anayetoka Bondo katika Kaunti ya Siaya pia alifunguka kuhusu uhusiano mzuri na muungano thabiti kati yake na watoto wa mwajiri wake.

Alisema alijisikia kukaribishwa sana alipokuwa na familia ya Lebanon kwani wote walimtendea vyema na walithamini kazi nzuri aliyowafanyia.

“Hapo nilijisikia kuwa nyumbani. Tofauti pekee ni mimi nilikuwa nalipwa. Ninawapenda watoto kwa sababu wanathamini kazi yangu na wananipenda kwa hilo. Walikuwa wakinichukulia kama mzazi wao,” alisema.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved