logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Biden amshambulia Trump kwa mara ya kwanza baada ya kuondoka Ikulu

Biden amekosoa sera za ustawi wa jamii katika utawala wa Trump kwenye hotuba yake ya kwanza tangu kuondoka madarakani.

image
na BBC NEWS

Kimataifa16 April 2025 - 15:22

Muhtasari


  • Biden aliuambia mkutano huko Chicago kwamba serikali imechukua "mwelekeo wa kikatili" katika Idara ya Ustawi wa Jamii.
  • Biden - ambaye alikuwa akizungumza katika hafla ya haki za walemavu - hakugusia kuondoka kwake kutoka Ikulu ya White.

The planned arms sale comes just over a fortnight before Biden leaves office/Screengrab

Aliyekuwa Rais wa Marekani Joe Biden amekosoa sera za ustawi wa jamii katika utawala wa Trump kwenye hotuba yake ya kwanza tangu kuondoka madarakani.

Rais huyo wa zamani wa Marekani aliuambia mkutano huko Chicago kwamba serikali imechukua "mwelekeo wa kikatili" katika Idara ya Ustawi wa Jamii, mfumo ambao Donald Trump na Elon Musk - ambaye anaongoza juhudi za kupunguza gharama za Ikulu ya White House - wamesema umekumbwa na udanganyifu.

Biden hakumtaja Trump kwa jina wakati wa hotuba yake siku ya Jumanne, lakini alisema: "Katika muda usiozidi siku 100, utawala huu mpya umefanya uharibifu mkubwa na mabaya mengi. Ni jambo la kusikitisha"

Biden - ambaye alikuwa akizungumza katika hafla ya haki za walemavu - hakugusia kuondoka kwake kutoka Ikulu ya White au uchaguzi wa rais wa 2024.

Wanasiasa wa chama cha Democratic wameushutumu mara kwa mara utawala kwa kupanga kupunguza ufadhili katika Idara ya Ustawi wa Jamii.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved