Picha hii iliyopigwa Oktoba 24, 2025 inaonyesha SUV mpya za mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, wakati wa hafla ya uzinduzi mjini Cape Town, Afrika Kusini. Mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, alizindua SUV zake mpya za mfululizo wa T hapa Ijumaa jioni, na kuvutia hamasa kubwa kutoka kwa watumiaji na kuonyesha umaarufu unaoongezeka wa chapa za magari ya China Afrika Kusini. (Xinhua/Han Xu)
Mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, alizindua SUV zake mpya za mfululizo wa T Ijumaa jioni katika uwanja wa Grand Parade mjini Cape Town, na kuvutia hamasa kubwa kutoka kwa watumiaji na kuonyesha umaarufu unaoongezeka wa chapa za magari ya China Afrika Kusini.
Hafla hiyo, iliyohudhuriwa na mamia ya wawakilishi kutoka vyombo vya habari vya ndani, maduka ya magari, washirika wa kibiashara na jamii, ilitambulisha miundo ya Jetour T1 na T2. Magari hayo yataanza kuuzwa katikati ya Novemba kupitia zaidi ya maduka 55 kote Kusini mwa Afrika.
Ilianzishwa mwaka 2018 kama chapa tanzu ya mtengenezaji wa magari wa China, Chery, Jetour inalenga SUV zinazochanganya muundo wa kuvutia, utendaji bora na teknolojia ya hali ya juu.
Ke Chuandeng, rais wa Jetour International, alisema mfululizo wa T tayari umepata sifa nje ya nchi.
“Tangu kuzinduliwa katika masoko mengine ya kimataifa, Jetour T1 na T2 zimepata sifa nzuri kutoka kwa watumiaji na wachambuzi sawa sawa. Katika eneo la Ghuba, hasa katika Umoja wa Falme za Kiarabu na Qatar, miundo hiyo miwili imekuwa vipenzi vya wakazi na nyota wa mitandao ya kijamii, ikionekana mara kwa mara barabarani Dubai na Doha,” alisema.
Aliongeza kuwa watumiaji wa Afrika Kusini wamekuwa wakingoja kwa muda mrefu uzinduzi huo. “Sasa miundo yote miwili inapatikana rasmi Afrika Kusini, na mrejesho wa awali umekuwa mzuri sana,” alisema.
Ke pia alitangaza kuwa Jetour itatoa magari 70 ya mfululizo wa T kwa matumizi wakati wa Mkutano ujao wa Kundi la Nchi Ishirini (G20) utakaofanyika Johannesburg mwishoni mwa Novemba.
Nic Campbell, makamu wa rais wa Jetour Afrika Kusini, alisema mwitikio wa soko umevuka matarajio.
“Tangu Jetour iingie katika soko la Afrika Kusini mwaka jana, kumekuwa na matarajio makubwa kwa mfululizo wa T. Tunafurahia kuzindua T1 na T2 kwa wakati mmoja leo, hatua ambayo tunaamini itabadilisha namna watu wanavyopata uzoefu wa SUV Afrika Kusini.”
“Tulipozindua mara ya kwanza Septemba 2024, mwitikio ulizidi matarajio yetu, na tunatarajia mapokezi makubwa zaidi kwa miundo hii mipya,” alisema.
Imani yao iliungwa mkono na watumiaji wa Afrika Kusini ambao wameona ongezeko la magari ya China barabarani.
Babalo Ndenze, mwandishi wa habari wa Afrika Kusini aliyeshuhudia hafla hiyo, aliita magari ya China “magari ya wakati huu.” “Yanafanya kazi vizuri, sawa tu na magari ya Kijerumani,” alisema.
Alitaja teknolojia na thamani kama faida kuu za magari ya China. “Ni ya kisasa sana kiteknolojia, hata yale ya ngazi ya kuingia sokoni. Magari ya China yana vifaa bora zaidi,” alisema, akibainisha kuwa “kwa upande wangu, kinachoyatofautisha magari ya China ni teknolojia.”
Ndenze aliongeza kuwa miundo ya China inazidi kuonekana kila mahali. “Kwa sasa yanaongoza kwa mauzo na umaarufu. Ukitazama popote uendapo, popote uendeshapo gari, unaona gari la China kila kona,” alisema.
Jessica Bartlett, mtumiaji mwingine wa eneo hilo ambaye amewahi kuendesha gari la China, alisema alivutiwa na ubora wake. “Kwa kweli ni mazuri sana, na nadhani yanachukua nafasi ya chapa kubwa.”
Marly Vivier, Msouth Afrika mwingine kijana ambaye aliwahi kumiliki gari la China, alikubaliana naye. “Kwa hiyo ninafuraha sana kuona uzinduzi wa T1 na T2, na ninafuraha kwa kila kitu kinachokuja mbele yetu.”
Vivier alisema mitazamo hasi kuhusu magari ya China ilikuwa inapotea kadri madereva wengi wanavyoyajaribu moja kwa moja, akibainisha kuwa gari la China alilowahi kumiliki “halikuwa na matatizo yoyote makubwa tangu mwanzo.”
Alisema uaminifu ni moja ya nguvu za magari ya China. “Nadhani kweli yatachukua nafasi kubwa, na ninayapenda hilo.”
Picha hii iliyopigwa Oktoba 24, 2025 inaonyesha SUV mpya ya mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, wakati wa hafla ya uzinduzi mjini Cape Town, Afrika Kusini. Mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, alizindua SUV zake mpya za mfululizo wa T hapa Ijumaa jioni, na kuvutia hamasa kubwa kutoka kwa watumiaji na kuonyesha umaarufu unaoongezeka wa chapa za magari ya China Afrika Kusini. (Xinhua/Han Xu)
Watu wakihudhuria hafla ya uzinduzi wa SUV mpya za mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, mjini Cape Town, Afrika Kusini, Oktoba 24, 2025. Mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, alizindua SUV zake mpya za mfululizo wa T hapa Ijumaa jioni, na kuvutia hamasa kubwa kutoka kwa watumiaji na kuonyesha umaarufu unaoongezeka wa chapa za magari ya China Afrika Kusini. (Xinhua/Han Xu)
Watu wakihudhuria hafla ya uzinduzi wa SUV mpya za mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, mjini Cape Town, Afrika Kusini, Oktoba 24, 2025. Mtengenezaji wa magari wa China, Jetour, alizindua SUV zake mpya za mfululizo wa T hapa Ijumaa jioni, na kuvutia hamasa kubwa kutoka kwa watumiaji na kuonyesha umaarufu unaoongezeka wa chapa za magari ya China Afrika Kusini. (Xinhua/Han Xu)
