Waimbaji wakitumbuiza wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. Fanuel Mulwa alikuwa na furaha tele baada ya kuwashinda washiriki kadhaa na kutwaa ushindi wa Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China lililozinduliwa Nairobi, mji mkuu wa Kenya, Novemba 2025. Msanii huyo alishiriki katika kila kipindi cha shindano hilo, akiwavutia majaji kwa sauti yake laini, kujiamini na uwezo mkubwa wa kutawala jukwaa. “Uzoefu ulikuwa mzuri, na wasanii walikuwa na ushindani mkubwa. Wakati wa usaili, niliimba wimbo uitwao Kwaheri — neno la Kiswahili linalomaanisha kuaga — kama njia ya kusonga mbele baada ya maumivu ya mapenzi ya awali,” Mulwa aliambia Xinhua kabla ya fainali.Kukutana na nguli wa muziki wa hapa nchini wakati wa usaili katika studio moja jijini Nairobi kulimpa hamasa, alisema, akiongeza kuwa moyo waliompa majaji ulimchochea kuimarisha kipaji chake na kulenga ushindi katika shindano lililowavutia watazamaji nchini Kenya na kwingineko.Mulwa alisema uzoefu huo uliboresha ujuzi wake wa uandishi wa nyimbo, na anapanga kutumia fedha za ushindi wa shilingi milioni moja za Kenya (takribani dola 7,700 za Marekani) kuanzisha studio ya kukuza kizazi kijacho cha vipaji vya muziki nchini. (Xinhua/Yang Guang)Fanuel Mulwa alikuwa na furaha tele baada ya kuwashinda washiriki kadhaa na kutwaa ushindi wa Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China lililozinduliwa Nairobi, mji mkuu wa Kenya, Novemba 2025.
Msanii huyo alishiriki katika kila kipindi cha shindano hilo, akiwavutia majaji kwa sauti yake laini, kujiamini na uwezo mkubwa wa kutawala jukwaa.
“Uzoefu ulikuwa mzuri, na wasanii walikuwa na ushindani mkubwa. Wakati wa usaili, niliimba wimbo uitwao Kwaheri — neno la Kiswahili linalomaanisha kuaga — kama njia ya kusonga mbele baada ya maumivu ya mapenzi ya awali,” Mulwa aliambia Xinhua kabla ya fainali, zilizofanyika Februari 1.
Kukutana na nguli wa muziki wa hapa nchini wakati wa usaili katika studio moja jijini Nairobi kulimpa hamasa, alisema, akiongeza kuwa moyo waliompa majaji ulimchochea kuimarisha kipaji chake na kulenga ushindi katika shindano lililowavutia watazamaji nchini Kenya na kwingineko.
Mulwa alisema uzoefu huo uliboresha ujuzi wake wa uandishi wa nyimbo, na anapanga kutumia fedha za ushindi wa shilingi milioni moja za Kenya (takribani dola 7,700 za Marekani) kuanzisha studio ya kukuza kizazi kijacho cha vipaji vya muziki nchini.
Ilizinduliwa Novemba 12 na Hunan TV International ya China kwa ushirikiano na chombo cha habari cha hapa nchini, Sing for Africa inalenga kukuza vipaji vya muziki vya vijana huku ikiimarisha mahusiano na urafiki wa kitamaduni kati ya China na Afrika.
Zaidi ya wasanii 500, akiwemo Mulwa, walihudhuria usaili wa awali mwishoni mwa Novemba. Mashindano yalifanyika kwa vipindi vitano, na kufikia kilele chake katika fainali za Februari 1.
Akiwa msanii mahiri wa neo-soul, Mulwa alisema onyesho hilo pia lilitoa jukwaa la kuimarisha mabadilishano ya kitamaduni kati ya China na Kenya yanayonufaisha wabunifu wa pande zote.
“Ninatazamia kushirikiana na wasanii wa Kichina. Tunaweza kuimba pamoja na hatimaye kuunda mabadilishano ya kitamaduni kupitia muziki,” alisema.
Kwa Mathew Munyiri, rapa anayejulikana kwa jina la kisanii ICCEY M, kushiriki Sing for Africa kuligeuka kuwa hatua muhimu, kikimpa mwangaza na malezi kutoka kwa wabobezi wa sekta hiyo.
“Hapo awali nilikuwa na wasiwasi kwa sababu nilikutana na marapa wenye vipaji vikubwa wakati wa usaili, lakini baadaye nikarejesha kujiamini. Nilipoitwa kushiriki fainali, nilifurahi sana,” alisema Munyiri, mmoja wa fainalisti watano.
Fainalisti mwingine, Duncan Mwangi, anayejulikana jukwaani kama Kalton 254, alisema kufika hatua za mwisho tayari ilikuwa hatua kubwa.
“Nilikuwa na furaha na pia wasiwasi kuhusu fainali. Rapa kufika fainali katika shindano hili tayari ni urithi,” alisema Mwangi, aliye katika umri wa mapema wa miaka ya 20.
Kutoka kwa takribani washiriki 500 katika usaili wa awali, ni 21 pekee waliopita hadi raundi zinazofuata, huku watano wakichaguliwa hatimaye kwa fainali kuu. Onyesho la vipaji na matukio yanayohusiana pia ni sehemu ya shughuli muhimu za kuadhimisha Mwaka wa 2026 wa Mabadilishano ya Watu kwa Watu kati ya China na Afrika.
Sammy Dee, mtayarishaji na mkurugenzi wa televisheni, alisema shindano hilo lilivutia kundi tofauti la wanamuziki kutoka katika mitindo kama neo-soul, hip-hop ya mijini na rhythm and blues. Watayarishaji walifanya kazi kwa karibu na washiriki, wakibaini waigizaji wenye ahadi lakini waliokuwa hawajulikani awali na kuwahimiza kuunda rekodi za asili zenye ubora wa juu.
“Tulitaka kutoa ubora wa juu zaidi kutoka kwa wasanii na pia tuliwahimiza kutunga nyimbo zao asilia. Maarifa waliyopata yatakuwa muhimu sana kwa mafanikio yao ya baadaye,” alisema Dee.
Aliongeza kuwa kufanya kazi bega kwa bega na wenzao wa Kichina katika onyesho la vipaji kulikuwa na mabadiliko makubwa, na kulimpa ujuzi mpya wa uzalishaji wa televisheni wenye matumaini makubwa kwa sekta ya ubunifu ya Kenya.
Motif Di Don, mkurugenzi wa muziki kutoka Kenya, alielezea shindano hilo kama mfano wa kulea vipaji vya kisanii vinavyoweza kuvuka mipaka ya kitamaduni na kijiografia. “Ikiwa tunaweza kutengeneza muziki unaovuka hadi China, itakuwa ajabu. Kuna watu wengi sana huko, na tunaweza kufikia hadhira kubwa ya usikilizaji mtandaoni,” alisema Motif.
Fanuel Mulwa anasherehekea na wengine baada ya kushinda Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 30, 2025. (Xinhua/Yang Guang)
Fanuel Mulwa akitumbuiza wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Yang Guang)
Waimbaji wakitumbuiza wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Yang Guang)
Fanuel Mulwa akitumbuiza wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Xie Jianfei)
Fanuel Mulwa akitumbuiza wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Yang Guang)
Fanuel Mulwa akitoa mahojiano wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Yang Guang)
Fanuel Mulwa akipiga gitaa nyumbani Kaunti ya Kajiado, Kenya, Januari 16, 2026. (Xinhua/Xie Jianfei)
Fainalisti wakisikiliza mrejesho wa majaji wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 30, 2025. (Xinhua/Xie Jianfei)
Watu wakitazama burudani wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Xie Jianfei)
Waimbaji wakitumbuiza wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Yang Guang)
Fanuel Mulwa (kushoto) akitoa mahojiano wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Xie Jianfei)
Majaji wakitoa mrejesho kwa washiriki wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Xie Jianfei)
Fanuel Mulwa (mbele) akisherehekea na wengine baada ya kushinda Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 30, 2025. (Xinhua/Xie Jianfei)
Fanuel Mulwa akitoa mahojiano wakati wa fainali za Sing for Africa, onyesho la vipaji vya muziki linaloungwa mkono na China jijini Nairobi, Kenya, Desemba 29, 2025. (Xinhua/Xie Jianfei)
Fanuel Mulwa (kushoto) akizungumza na marafiki nyumbani Kaunti ya Kajiado, Kenya, Januari 16, 2026. (Xinhua/Xie Jianfei)
Fanuel Mulwa akifanya mazoezi ya kuimba nyumbani Kaunti ya Kajiado, Kenya, Januari 16, 2026. (Xinhua/Xie Jianfei)


