logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kush Tracey afunguka sababu ya kuchubua ngozi yake, kwa nini aliacha na pesa alizotumia

Tracey alifichua kuwa alianza kuchubua ngozi yake takriban miaka sita iliyopita.

image
na Radio Jambo

Habari26 October 2023 - 08:31

Muhtasari


•Tracey alisema hamu yake ya kufanya majaribio na chaguo lake la marafiki ziliathiri sana uamuzi wake wa kubadilisha rangi ya ngozi yake.

•Tracey alifichua kuwa alianza mchakato wa kurejea katika ngozi yake ya kawaida baada ya kuona hakuna maana ya kujichubua tena.

ndani ya studio za Radio Jambo.

Mtayarishi wa Maudhui maarufu wa Kenya Kush Tracey amefunguka kuhusu safari yake ya mabadiliko ya ngozi tangu alipoanza kujichubua hadi alipogundua kuwa si sawa, akaacha na kuanza kurejea kwenye ngozi yake ya kawaida nyeusi.

Katika mahojiano na mtangazaji Massawe Japanni kwenye Radio Jambo, mwanamuziki huyo wa zamani alifichua kuwa alianza kuchubua ngozi yake takriban miaka sita iliyopita.

Tracey alisema kuwa hamu yake ya kufanya majaribio na chaguo lake la marafiki ziliathiri sana uamuzi wake wa kubadilisha rangi ya ngozi yake.

“Nilianza kujichubua mwaka wa 2017. Nilifanya majaribio sana. Sijui mbona nilikuwa na upuuzi. Nilikuwa nasema niko mweusi sana. Nilikuwa na marafiki ambao walikuwa wanajichubua. Nadhani marafiki zangu walikuwa na ushawishi mkubwa katika maamuzi niliyokuwa nikifanya,” Kush Tracey alisema.

Aliendelea kufichua kiasi kikubwa cha pesa ambacho alitumia katika miaka minne ambayo alijaribu kugeuza ngozi yake kutoka nyeusi hadi nyeupe.

Pia alizungumza kuhusu jinsi alivyojaribu njia mbalimbali za kujichubua ngozi, zote katika jitihada za kupata matokeo bora haraka iwezekanavyo.

“Mara ya kwanza nilipoinunua ilikuwa 40,000. Nilizipakia kwenye gari langu. Ziliibiwa. Nilikwenda kununua zaidi na kuanza kujichubua. Iliendelea kwa takriban miaka 3-4. Nilijaribu sindano, vidonge, poda. Kila wiki naenda kudungwa sindano moja. Ni 45,000 kwa mwezi. Poda iliuzwa kwa wiki mbili,” alisema.

Mzungumzaji huyo wa mabadiliko alisema kwamba hana uhakika sana kuhusu kiasi halisi cha pesa alichotumia kwenye kujichubua lakini akadokeza kuwa ni kama mamilioni kadhaa.

“Sijui pesa nilitumia. Siwezi kusema. Kuna wakati nilikuwa naona bidhaa fulani inachelewa na ningejaribu kitu kingine. Nilikuwa nikiona wasichana wenye ngozi nyeusi wakiwa wazuri. Nilikuwa nikishangaa ni nini maana ya mimi kupauka,” Kush Tracey alisema.

Tracey alifichua kuwa alianza mchakato wa kurejea katika ngozi yake ya kawaida baada ya kuona hakuna maana ya kujichubua tena.

“Mbali na upande wa pesa, nilianza kuuliza kuna umuhimu gani. Pia nimekuwa na mabadiliko mengi. Ngozi yangu ilirudi. Niliamka siku moja nikasema sifanyi chemistry kwa akili yangu, nilienda kwenye mafuta asilia tu,” alisema.

Alisema alipokuwa akichubua ngozi yake, alikuwa na umri wa miaka ya mapema na katikati 20s.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved