logo

NOW ON AIR

Listen in Live

David Luiz apungia Arsenal kwaheri

Difenda David Luiz amewaaga mashabiki na wachezaji wenzake kwaheri baada ya kushiriki mazoezi yake ya mwisho na klabu ya Arsenal

image
na Radio Jambo

Mahakama22 May 2021 - 18:55

Muhtasari


•Difenda David Luiz amewaaga mashabiki na wachezaji wenzake kwaheri huku baada ya kushiriki mazoezi yake ya mwisho na klabu ya Arsenal

David Luiz

Difenda wa timu ya Arsenali David Luiz amewaaga mashabiki na wachezaji wenzake kwaheri.

Hii ni kutokana ya mkataba wake na klabu hiyo ya London kutarajiwa kuisha mwisho wa msimu huu. Luiz alikuwa na mkataba wa miaka miwili na klabu hiyo ya gunners.

Raia huyo wa Brazil alijiunga na klabu ya Gunners mwakani 2019 akitokea klabu hasidi ya Chelsea.

Siku ya Jumanne, klabu ya Arsenali ilitangaza kuwa ilikubaliana kutompa mchezaji huyo wa miaka 34 mkataba mwingine huku kocha mkuu Mikel Arteta akimsifia sana Luiz.

"Amesaidia sana, ni mtu tunayempenda na kumthamini sana kwa hivyo nasema tu asante na kumtakia kila la heri katika sura yake ijayo"  Arteta alisema.

Siku ya Jumamosi Luiz alishiriki mazoezi yake ya mwisho na klabu hiyo ya Arsenal huku akiwaaga wachezaji na mashabiki kwaheri na kuwashukuru kwa ushirikiano.

Luiz ameendelea kupokea jumbe za kheri njema kutoka kwa mashabiki na wachezaji mbalimbali.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved