logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Rayvanny amwaga machozi ya furaha akiwashukuru Wakenya kufanya wimbo wake namba moja

Rayvanny alionekana kurudiana na Fayhma aliyetengana naye mwaka wa 2020.

image
na

Mahakama04 April 2023 - 06:16

Muhtasari


• Video hiyo ya Rayvanny ambaye alimshirikisha mama mtoto wake kama Vixen ilitoka wikendi iliyopita na kupata mapokezi makubwa.

•Mpaka sasa, wimbo huo una watazamaji zaidi ya milioni moja kwenye jukwaa la YouTube chini ya siku tatu.

Rayvanny na Fahyvanny wakioneshana mahaba mazito baharini kwenye boti.

Msanii wa Bongo,Raymond Mwakyusa almaarufu Rayvanny amefichua kuwa wakati mwingine anajihisi kama Mkenya.

Hili linajiri baada ya mashabiki w wake wa Kenya kumfanya nambari moja katika wimbo wake na aliyekuwa mpenzi wake Fayvanny kwenye mtandao wa You Tube hivyo kumfanya msanii huyo kueleza furaha yake kwa uungwaji mkono ambao Wakenya wanampa.

Rayvanny vile vile aliwashukuru mashabiki wake wa Tanzania kwa kuwa pia alikuwa anaongoza kwenye majukwa na chati ya Daily chats huku akionyesha kuwa anawaenzi watanzania pia kwa upendo wao kwake

"Aki kuna muda huwa najiona Mkenya kabisa,,Forever nafasi ya 1 Kenya.... nambari 1 Tanzania kwenye Daily Charts," alisema Rayvanny.

Video ya Wimbo wake wa Forever imefikisha watazamaji milioni 1.2 ndani ya siku mbili.

Rayvanny hivi majuzi walirudiana na aliyekuwa mpenzi wake Fahyvanny baada ya kutengana kwa miaka mitatu.

Hili lilidhihirika walipotoa kibao cha Forever pamoja naye huku akiahidi kumpenda Fahyvanny daima kwenye wimbo huo.

Rayvanny alimmiminia sifa mpenzi wake kwa  urembo wake asilia na kusema kuwa atakuwa kando yake kila wakati.

Rayvanny na Fahyvanny waliwachana mwaka wa 2020 kisha Vanny akachumbiana na mwana wa Fridah Kajala, Paula Kajala.

Hata hivo, walipata matatizo katika mahusiano yao baada ya madai kuwa Harmonize alimmezea mate Paula ilhali alikuwa kwenye mahusiano na mamake ambaye ni Frida.

Fahyma alimshutumu Rayvanny kwa kutojali familia .

Mashabiki wa Rayvanny walifurahia wimbo wao na kuchumbiana kwa Rayvanny na Fahyma kwa mara nyingine


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved