logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mlanguzi wa dawa za kulevya afungwa jela miaka 40

Vile vile, mahakama imeamuru mshukiwahuyo kulipa faini ya shilingi milioni 600

image
na Brandon Asiema

Mahakama19 November 2024 - 14:53

Muhtasari


  • Mshukiwa alishtakiwa pamoja na mume wake ila kesi ilibadili mkondo wa kutupilia mbali kesi dhidi ya mumewe baada ya kuaga dunia siku 9 baada ya kuripotiwa kupotea.
  • Wakati wa kutoa hukumu mahakama ilibaini kuwa hakukuwa na upungufu katika ushahidi uliowasilishwa mahakamani wa kudai kuwa dawa hizo za kulevywa zilipandikizwa nyumbani kwa mshukiwa.

Court gavel/FILE

Kurugenzi wa mashtaka ya umma (DPP) imeshinda kesi dhidi ya mwanamke aliyeshtakiwa kwa madai ya kuhusika katika ulanguzi wa dawa za kulevya katika jiji la Mombasa

Katika hukumu iliyosomwa na hakimu David Odhiambo kwa niaba ya hakimu Martin Rabera, mshukiwa alipatikana na hatia ya ulanguzi wa heroine ya kilo 91.738  mnamo Septemba 20, 2018 katika mtaa wa Kikambala kwenye kaunti ya Kilifi. Herione hiyo kwa mujibu wa ushahidi uliowalishwa mbele ya mahakama hiyo iligharimu shilingi milioni 275.214.

Upande wa mashtaka ukiongozwa na Barbara Sombo, ulieleza mahakama kuwa dawa hiyo ya kulevya ilikuwa imewekwa katika masanduku mawili ya rangi ya kahawia na mfuko mmoja mdogo ikiwa katika hifadhi kwenye nyumba moja.

Hakimu Rabera alisema kuwa upande wa mashtaka uliwasilisha ushahidi wa kutosha ikiwemo ushuhuda kutoka kwa maafisa ambao waliendesha msako katika makao ya mshukiwa.

Aidha kesi ilichukua mkondo tofauti wa kutupilia mbali mashtaka dhidi ya mume wa mshukiwa baada ya kuaga dunia. Mshukiwa alishtakiwa pamoja na mumewe aliyejulikana maarufu kama Kandereni ila aliaga siku tisa baada ya kuripotiwa kupotea kwa njia zisizoeleweka.

Akitoa hukumu hiyo, hakimu Rabera alisema kuwa hakukuwa na upungufu katika ushahidi uliowasilishwa mahakamani wa kudai kuwa dawa hizo za kulevywa zilipandikizwa nyumbani kwa mshukiwa.

“Hakuna mianya katika ushahidi wa kuonyesha kwamba dawa hizo zilihitilafiwa ama kuweka, baada ya kupitia na kuchambua ushahidi, Napata mashtaka dhidi ya mshukiwa kuwa ukweli bila ya shaka yoyote.” Alisema hakimu Rabera katika hukumu yake.

Aidha mshukiwa vile vile ametakiwa kulipa faini ya shilingui milioni 600.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved