logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Covid-19:26 waaga dunia,1,463 wapatikana na corona

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 126,170  kutoka kwa sampuli 1,443,701

image
na Radio Jambo

Michezo25 March 2021 - 14:10

Muhtasari


  • Watu 26 waaga dunia kutokana na corona,huku 121 wakiwa ICU
  • Pia 1,463 wapatikana na corona ilhali 498 wameona maradhi hayo

Kenya imerekodi visa 1,463 vipya vya maambukizi ya COVID-19 kutoka kwa sampuli 8,976 katika muda wa saa 24 zilizopita.

Kufikia sasa Kenya imesajili jumla ya visa 126,170  kutoka kwa sampuli 1,443,701

Katika visa hivi vipya, 1428 ni raia wa Kenya huku 35 wakiwa raia wa kigeni, 802 ni wa kiume na 661 ni wanawake.

 

Mgonjwa mwenye umri wa chini ana miezi tatu huku mwenye umri wa juu akiwa na miaka 103.

Kulingana na takwimu za wizara ya afya watu 498 wamepona virusi vya corona, 372walipona wakiwa nyumbani huku 126 wakipona wakiwa katika hospitali mbali mbali, na kufikisha idadi jumla ya 91,268 ya watu waliopona.

Hata hivyo habari za kuhuzunisha ni kwamba watu 26 waliaga dunia kutokana na maambukizi kufikisha 2,096watu waliofariki kutokana na maambukizi ya virusi vya corona.

Jumla ya wagonjwa 1,080 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya , huku 3,825wakiuguzwa nyumbani.

Wagonjwa 121 wamo katika kitengo cha wagonjwa mahututi (ICU)

 

 

 

 

 

 

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved