logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wacha kujificha kwa neno kosa ukipatikana ukidanganya-Nadia Mukami

ujumbe ambao wanamitandao wamedai kwamba kunaweza kuwa shida katika uhusiano wake

image
na Radio Jambo

Habari10 September 2021 - 10:40

Muhtasari


  • Soma ujumbe wake Nadia Mukami uliozua mdahalo mitandaoni
nadia-mukami-341

Huku wakiwa Marekani katika  ziara ya muziki katika majimbo tofauti Nadia Mukami na mpenzi wake Arrow Bowy wamekuwa pamoja  tangu walipojitokeza na kutangaza hadharani mapenzi yao kwa kila mmoja ambayo wanamtandao wanafikiria inaweza kuwa inakabiliwa na shida kwa sasa.

Nadia ameibua mdahalo mitandaoni  baada ya kuchapisha maandishi ya kifiche juu ya mambo ya kudanganya kuwalaumu wote ambao huiita ni makosa.

Ni ujumbe ambao wanamitandao wamedai kwamba kunaweza kuwa shida katika uhusiano wake Nadia na Arrow Bowy.

"Makosa ni ajali Kudanganya na kusema uwongo sio makosa., Ni chaguo za kukusudia. Acha kujificha nyuma ya neno kosa ukikamatwa ukidanganya ... " Aliandika Nadia.

Baada ya wawili hao kufichua uhusiano wao wamekuwa wakipkea kejeli kutoka kwa mashabiki huku baadhi yao wakiwapongeza.

Je kunaweza kuwa na shida kati ya uhusiano wa wawili hao au ni kiki tu, kama vile wasanii wengi hufanya ili kupata wafuasi wengi mitandaoni.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved