logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Atafute bibi, nyumba yake chafu inahitaji mwanamke!" Mr Seed ampasha Ringtone baada yake kumkosoa

Mr Seed alisema muda umewadia Ringtone kutafuta mke huku akimshtumu kwa kushindwa kutunza nyumba yake.

image
na Radio Jambo

Makala03 January 2022 - 09:07

Muhtasari


•Mr Seed alisema muda umewadia Ringtone kutafuta mke huku akimshtumu kwa kushindwa kutunza nyumba yake.

•Aliwahakikishia mashabiki wake kwamba hajagura injili kama alivyodai Ringtone.

Mr Seed, Ringtone Apoko

Mwanamuziki wa nyimbo za injili Moses Tarus Omondi almaarufu kama Mr Seed amemkosoa sana mwenzake Ringtone Apoko kwa kumbandika jina  'mkubwa wa washerati' baada yake kutoa wimbo wa mapenzi.

Alipokuwa anahutubia wanahabari hivi majuzi, Mr Seed alisema Ringtone hafai kunyooshea wengine vidole na kudai kwamba amekuwa akinyemelea wanadada wengi hapa nchini.

Mr Seed alisema muda umewadia Ringtone kutafuta mke huku akimshtumu kwa kushindwa kutunza nyumba yake.

"Yeye ndiye mkubwa wa Washerati. Ringtone hakosi kwa DM ya msichana yeyote hii Nairobi. Aache kushinda amenyoosheana vidole, kwanza atafute bibi aoe. Juzi niliona mmekuwa kwa nyumba yake, nyumba chafu inahitaji mwanamke. Jokovu limeoza, microwave imeoza, anapika sukuma. Mwambieni atafute bibi 2022 atulie. Bibi atamueka laini, hii mdomo ako nayo hatakuwa nayo. Atakuwa anaongea hivi anakumbuka akirudi kwa nyumba atapigwa. Huyo anaweza kaliwa na mwanamke!" Alisema Seed.

Mr Seed aliwahakikishia mashabiki wake kwamba hajagura injili kama alivyodai Ringtone. Alisema angali anasambaza maneno mazuri kupitia kwa muziki wake.

"Wokovu ni binafsi kwa kila mtu. Mimi ni msanii, mimi ni msanii wa injili, bado nasambaza wema. Ama Ringtone akienda kutafuta mwanamke atasema Mungu ameniambia wewe ndio bibi yangu? Hawezi! Nina hakika hao wasichana wake huwa anawachezea 'Dawa ya baridi' hapo" Seed alisema.

Alisema kwamba amejitolea kumsaidia Apoko kwa kufanya collabo naye ili angalau apate kazi ya kufanya aache udaku.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved