logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii Eko Dydda kuwania kiti cha MCA Mathare kaskazini

Mwimbaji huyo hakutaja ikiwa atajiunga na chama cha kisiasa kabla ya uchaguzi.

image
na Radio Jambo

Makala26 January 2022 - 09:58

Muhtasari


  • Msanii Eko Dydda kuwania kiti cha MCA Mathare kaskazini

Msanii na rappa maarufu Emmanuel Dydda almaarufu Eko Dydda, ametangaza kuwania kiti cha MCA Mathare Kskazini.

Katika siku za hivi majuzi tumewaona na kushuhudia wasanii na watangazaji mbali mbali wakijiunga na ulingo wa siasa kuwania viti tofauti katika uchaguzi mkuu wa Agosti.

Dydda alieleza kuwa alichagua kukabiliana na changamoto hiyo baada ya kuwa raia asiyeridhika kwa muda mrefu.

Akipendekeza kuwa viongozi waliochaguliwa wameendelea kukatisha tamaa taifa, mwimbaji huyo wa Niko Na Reason alisisitiza kuwa Uchaguzi Mkuu ni fursa kwa sera kujirekebisha.

Mwimbaji huyo hakutaja ikiwa atajiunga na chama cha kisiasa kabla ya uchaguzi.

Tangazo hilo lilipongezwa na wasanii wenzao Holy Dave na Kriss Erroh ambao waliahidi kumuunga mkono mwenzao.

"Tumesema wabadilishe na maybe hawaoni kitu ya kubadilisha, so itabaki tujibadilishie inchi wenyewe, chukua kura sasa tubadilishe hizi mtaa KIMANGOTOS KIMANGOTOS hatulegezi kamba. MIK CULTURE love culture everywhere," Alisema Eko Dydda.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved