logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Uwoya: Si kwamba hatupati shida, wanaotusaidia hawatutangazi

Irene Uwoya anasema kila mtu hupata shida bali wengine hawatangazwi wanaposaidiwa.

image
na Radio Jambo

Makala09 March 2022 - 07:54

Muhtasari


• Irene Uwoya anasema kwamba kila mtu hupata shida ila wengine hawajulikani kama wanapata shida kwa sababu wanaowasaidia hawawatangazi.

Staa wa Bongo Movie Irene Uwoya anahisi kwamba siku hizi ni ngumu sana upate mtu anayetoa msaada bila kutangaza ama kwa maneno au katika video haswa katika hiki kizazi cha TikTok na WhatsApp ambapo kila tukio linarekodiwa.

Uwoya anasema kwamba kila mtu anahitaji msaada hata wao ambao wanaonekana mastaa na kudhaniwa na wengi kwamba pengine hawawezi kuwa na hitaji la kimsaada kutoka kwa watu wengine.

Ila pia staa huyo alichora tofauti inayojitokeza kati ya watu wanaotoa msaada na kusema kwamba kila mtu kwa sababu moja au nyingine huhitaji msaada lakini kinachofanya wengine wao wasijulikane ni kwa sababu wanawapa msaada hawana hulka ya kutangaza.

Sio kwamba hatupatagi shida ila wanaotusaidia hawatutangazi,” aliandika Uowya kwenye Instagram yake.

Katika kile alionekana kuweka kwenye mizani suala la Aristote kumchamba Wema Sepetu kwamba hana gari, Uwoya alikuwa na maana kwamba kila mtu ana nafasi yake katika maisha na kula watu ambao anawategemea kwa kumsaidia kutatua shida fulani ambazo mwenyewe hawezi kuzitatua.

Aidha wafuasi wake walimtaka afafanue zaidi huku wengine wakichukua kauli hiyo na kuanza kuichambua kwa uelewa wao binafsi.

“Hujawahi saidiwa na Aristote wewe, ungejuta,” aliandika shabiki kwa jina Babykher.

Je, unahisi kusaidia mtu halafu tukio hilo lichukuliwe kwa kamera na baadae kupakiwa kwenye mitandao ni vibaya ama ni haki?


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved