logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bishop Wanjiru ajiondoa kwenye kinyang'anyiro cha ugavana Nairobi, kumuunga mkono Sakaja

Wanjiru sasa atawania useneti kwa tikiti ya UD

image
na

Makala09 April 2022 - 15:25

Muhtasari


•Karen Nyamu pia alijiuzulu nafasi yake ya useneta na sasa atamuunga mkono Seneta maalum Millicent Omanga kuwania kiti hicho.

Askofu Margaret Wanjiru wa kanisa la Jesus is Alive Ministry ametangaza kuwa ameacha azma yake ya kuwania kiti cha Ugavana wa Nairobi.

Wanjiru alitangaza kujiondoa kwenye kinyang'anyiro hicho ili kumwachia Seneta Johnstone Sakaja ambaye sasa ndiye atakayepeperusha bendera ya UDA.

Alikuwa anazungumza baada ya mkutano ulioandaliwa katika makazi rasmi ya DP Ruto mtaani Karen. Wanjiru sasa atawania useneti kwa tikiti ya UDA.

"Ninataka wafuasi wetu na wanachama wote wa chama waelewe, na hata viongozi wetu wengine wote wa chama waelewe kwamba muungano huja na changamoto kadhaa. Na mojawapo ya changamoto hizo ni kwamba lazima kuwe na kupewa na kupokonywa," Wanjiru alisema.

Katika matamshi yake, Sakaja alimsifu Wanjiru kwa kuchukua uamuzi huo mkubwa wa kujiuzulu na kuunga mkono azma yake.

Karen Nyamu pia alijiuzulu nafasi yake ya useneta na sasa atamuunga mkono Seneta maalum Millicent Omanga kuwania kiti hicho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved