logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wema Sepetu afunguka kuhusu ugomvi wake na Amber Lulu

Kulichimbuka wasiwasi kuhusiana na uhusiano wa wasanii hao baada yao kuonekana wakivurutana

image
na Radio Jambo

Makala27 April 2022 - 04:38

Muhtasari


•Wema alidhirisha kuwa kwa sasa uhusiano wake na Lulu ni mzuri huku akiwasihi watu wengine kutoingilia uhusiano wao.

Wema Sepetu na Amber Lulu

Mwigizaji Wema Sepetu ameweka wazi kuwa hakuna ugomvi wowote kati yake na mwanasoshalaiti Amber Lulu.

Siku chache zilizopatana kulichimbuka wasiwasi kuhusiana na uhusiano wa wasanii hao baada yao kuonekana wakivurutana siku kadhaa zilizopita.

Akizungumzia hayo, Wema amesema drama zilitokea baada  yake na 'Drama Queens' wenzake kukosa kutofautiana kuhusu masuala yao ya ndani.

"Ilikuwa tu ni kutoelewana  baina yangu na wenzangu. Lakini mliona tulikaa sawa. Tumeshapatana. Maisha yanaendelea na mipango ya kazi ipo mingi," Wema alisema katika mahojiano na wanahabari.

Wema alidhirisha kuwa kwa sasa uhusiano wake na Lulu ni mzuri huku akiwasihi watu wengine kutoingilia uhusiano wao.

"Tuko vizuri kabisa. Alafu Lulu ni mdogo wangu. Yule nikiamua namshika nampiga vibaya namwambia tulia. Nyinyi mkiona tukigombana msishadidie. Watu washike jembe wakalime. Kugombana ni vitu vya kawaida. Tunaweza tukagombana mkaingilia mkaja kuona aibu nyinyi mwishowe," Alisema.

Mwigizaji huyo alitangaza kuwa kuna shoo inayoandaliwa ambayo itamhusisha yeye pamoja na Irene Uwoya, Amber Lulu, Kajala Masanja, Auntie Ezekiel na Jacquline Wolper.

Sita hao wamejibandika majina 'Drama Queens' na 'Big Six'. Wamewasihi mashabiki kuwapokea ni kuunga mkono kazi zao. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved