logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nina bahati sana kuwa baba yako," Harmonize amsherehekea bintiye kwa ujumbe maalum

Zuuh Konde ametimiza miaka mitatu.

image
na Radio Jambo

Habari30 May 2022 - 17:33

Muhtasari


•Akisherehekea siku ya kuzaliwa ya bintiye, Harmonize alibainisha kuwa anajivunia sana kuwa baba yake Zuuh. 

•Shanteel alisema anajivunia sana Zuuh kuwa bintiye na kumhakikishi kujitolea maisha yake ili kumpa upendo usio na kikomo.

Binti wa pekee wa staa wa Bongo Harmonize, Zurekha Nasra almaarufu Zuuh Konde ametimiza miaka mitatu.

Zuuh ambaye ni mtoto wa Harmonize na Official Nana Shanteel aliadhimisha siku yake ya kuzaliwa Jumapili.

Akisherehekea siku ya kuzaliwa ya bintiye, Harmonize alibainisha kuwa anajivunia sana kuwa baba yake Zuuh. 

Harmonize alimtaja Zuuh kama rafiki wake wa dhati na kumhakikishia kuhusu upendo wake mkubwa kwake.

"Nakupenda sana rafiki yangu bora. Nina bahati sana kuwa baba yako. Kheri njema za kutimiza miaka mitatu kipenzi changu @zuuh_konde. Mungu akubariki," Harmonize alimwambia bintiye kupitia Instagram.

Bosi huyo wa Konde Music Worldwide aliambatanisha ujumbe wake na picha zinazoonyesha akiwa amembeba bintiye mikononi mwake.

Mamake Zuuh pia alimtakia kheri za siku ya kuzaliwa na kusema kuwa yeye  ni msukumo mkubwa kwake.

Shanteel alisema anajivunia sana Zuuh kuwa bintiye na kumhakikishi kujitolea maisha yake ili kumpa upendo usio na kikomo.

"Siku uliyozaliwa ilikuwa wakati mkubwa zaidi maishani mwangu!! Wakati unaenda haraka sana, juzi tu hungeweza kusimama na sasa napata kukuona ukikimbia! Nina bahati sana kwamba nilibarikiwa kupata binti mzuri kama wewe.. Wewe ni msukumo kwangu na natumai unahisi kuzungukwa na upendo na joto kwenye siku yako ya kuzaliwa. Nakuahidi kuwa nitajitolea maisha yangu yote kukupa upendo usio na kikomo. Heri ya kuzaliwa mpenzi wangu," Shanteel alimwandikia bintiye kupitia Instagram.

Desemba 2020 Harmonize alifichua kwamba alijitokeza kumfichua Zuuh na kukiri kuwa alimpata nje ya ndoa. Alisema alikuwa amemficha bintiye kwa zaidi ya miezi saba kwa kuhofia kuvunja ndoa yake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved