logo

NOW ON AIR

Listen in Live

“Alfajiri njema, nguvu mpya na safari inaendelea,” Willis Raburu asema baada ya kunyoa rasta

“Alfajiri njema, nguvu mpya na safari inaendelea,” Willis Raburu aliandika

image
na Radio Jambo

Makala06 August 2022 - 12:59

Muhtasari


• Willis Raburu anajiunga na wengine walionyoa rasta kama Nick Odhiambo, Thee Pluto, Magix Enga, Sean Andrew miongoni mwa wengine.

Mtangazaji Willis Raburu katika muonekano mpya bila rasta

Mtangazaji maarufu nchini, Willis Raburu hatimaye amezikata rasta zake alizodumu nazo kwa takribani miaka mitatu.

Katika picha ambayo aliipakia kwenye ukurasa wake rasmi wa Facebook, kinara huyo wa kipindi cha runingani cha 10Over10 alipakia picha hiyo huku akidokeza kwamab ndio tena amerudi mwanzo kuanza upya na kusonga mbele.

“Alfajiri njema, nguvu mpya na safari inaendelea,” Willis Raburu aliandika kwenye picha hiyo ambayo aliiweka kama utambulisho wake kweney mtandao wa Facebook.

Mashabiki wake walimsifia kwa muonekano huo mpya huku wakimuambia sasa anaonekana kaboreshwa na utanashati hata zaidi kuliko awali alipokuwa na chokodindo hizo kichwani.

Wengine wenye dhana ya kuhusisha rasta na dawa ya kulevya ya bangi walimwambia kwamba sasa ako vizuri na Wajackoyah amemtoka kichwani, kwa maana kwamba wakili msomi George Wajackoyah anayegombea urais ameupa upanzi na ukuzaji wa bangi kipaumbele katika manifesto yake.

“Muonekano ni mwepesi bila Dreadlocks, Wajakoyah ametoka kichwani mwako,” shabiki wake kwa jina Mitch Marya alimuambia.

“Yaani uliamua kuangusha Wajackoyah chini hivo tu!” mwingine kwa jina Tasha Baibe alimtania.

Raburu sasa anajiunga kweney orodha ndefu ya watu maarufu waliotangaza kuasi chama cha rasta akiwemo mtangazaji mwenye sauti nzito Nick Odhiambo ambaye alikuwa mpenzi wa nywele hizo kwa muda mrefu lakini miaka michache iliyopita akawashangaza wengi baada ya kuibuka na muonekano mpya wa nywele fupi.

Mjukuu wa rais wa tatu hayati Mwai Kibaki, Sean Andrew pia naye mapema mwaka huu kabla ya kifo cha babu yake alitangaza kuzinyoa rasta zake kwa kile alisema kwamba ni watu walikuwa wanamhusisha na dhana mbaya inayohusisha wapenzi wa rasta na visa hasi katika jamii kama kutumia bangi na kuhusishwa na magenge ya uhalifu kama Mungiki.

Wiki chache zilizopita pia mtayarishaji wa muziki wa gengrtone maarufu nchini Kenya, Magix Enga alipakia video kwenye ukurasa wake wa Instagram akisema kwamab ameamua kuachana na ufugaji wa nywele ndefu na ni wakati sasa wa kufanya kichwa kiwe laini bila hata mzizi mmoja wa nywele.

Katika orodha hiyo, Raburu pia anakutanqa na mkuza maudhui Thee Pluto ambaye naye aisema alizinyoa baada ya kuahidiwa kiasi cha pesa fulani na rafiki wake.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved