logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Wafungwa wanataka rais mpya awasamehe

Tunatumikia vifungo vya muda mrefu hapa na tunaamini kuwa atakayeshinda urais atatukumbuka. Hapo zamani, huruma ya rais ilipuuzwa na tunatarajia kwamba wengi watasamehewa miaka ijayo," Wafungwa hao walisema

image
na Radio Jambo

Makala09 August 2022 - 16:33

Muhtasari


•Wapiga kura wa Gereza Kuu la Nakuru wanamtaka rais mpya atakayechaguliwa kuwasamehe kupitia uwezo wa rais wa huruma  kuwasamea wafungwa.


Picha ya gereza ya Kamiti

Wapiga kura wa Gereza sasa  wanamtaka rais mpya atakayechaguliwa kuwasamehe kupitia uwezo wa rais wa huruma  kuwasamea wafungwa.

Wafungwa katika Gereza kuu la Nakuru pia walishiriki katika zoezi hilo la kitaifa.

Wakizungumza baada ya kupiga kura siku ya Jumanne, wafungwa hao walisema msamaha wa rais wakati mwingine hupuuzwa na wale wanaopaswa kuufanyia kazi, wakitoa wito kwa rais mpya kurahisisha mchakato huo.

 

“Tunatumikia vifungo vya muda mrefu hapa na tunaamini kuwa atakayeshinda urais atatukumbuka. Hapo zamani, huruma ya rais ilipuuzwa na tunatarajia kwamba wengi watasamehewa miaka ijayo," Wafungwa hao walisema wakiongea na moja ya vyombo vya habari hapa nchini.

 

Mwangalizi kutoka Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa, David Mwaura, alisema zoezi la upigaji kura katika kituo hicho lilikuwa la amani na utulivu.

"Tumeshuhudia uchaguzi wa amani na ulioendeshwa vyema na IEBC lakini ningependa kusisitiza kuhusu mafunzo ya Maajenti. Maajenti wengi hawajui kile kinachohitajika kwao," Mwaura alisema.

Kwingineko ni kwamba kulikuwa na mkanganyiko katika Gereza la Kati la Kibos (B) huko Kisumu ambapo upigaji kura kwa wafungwa ulichelewa sana.

Afisa msimamizi Evans Owili alisema wana wapiga kura 15 waliojiandikisha katika kituo cha kupigia kura lakini kuchelewa kwa hiyo zoezi si kwa mnajili  KIEMs wala sajili ya mwongozo.

 

Maarufu Zaidi

RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2026. All rights reserved