logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Christina Shusho hatimaye azungumzia kitendo cha Harmonize kuibusu miguu yake

Wawili hao walikutana nchini Kenya wikendi iliyopita kabla ya Harmonize kubusu miguu yake.

image
na Radio Jambo

Habari15 December 2022 - 07:26

Muhtasari


• Christina Shusho alimtaja Harmonize kama mwanake na kumtakia mema yatokayo kwa Mungu.

• Harmonize kwa upande wake alimuombea Shusho kufunikwa kwa damu ya Mungu siku zote.

Harmonize na Shusho

Mwimbaji wa Injili kutoka Tanzania Christina Shusho hatimaye amevunja kimya kuhusu kitendo cha msanii wa nyimbo za dunia Harmonize kuinama chini na kubusu miguu yake.

Wawili hao walikutana Kenya, jijini Eldoret na Harmonize alifanya kufuru kwa kupiga magoti chini na kuibusu miguu ya Shusho kwa furaha huku akimtaja kama mtumishi wa Mungu mmoja ambaye ni wa kweli kuwahi kutokea.

Mengi yalisemwa kuhusu kipande hicho cha video baadhi wakisema kuwa Harmonize ana njama fiche ya kuvunja ndoa ya Shusho kwani kitendo hicho ni cha kimahaba zaidi.

Lakini Shusho ameamua kufunguka kuhusu video hiyo na kumtaja Harmonize kuwa kijana mwadilifu anayeipambania Sanaa ya Tanzania.

Alisema hivi karibuni atafunguka kwa kina kiini cha mazungumzo yao ambayo walikuwa nayo baada ya kukutana wote Kenya, japo kuwa kila mmoja alikuwa anafukuzia shoo yake tofauti.

Nikiwa Kenya kwenye huduma nilifurahi kukutana na Mtanzania mwenzangu Naye kaja kupeperusha bendera ya Tanzania nchini Kenya. Tuliyo Yaongea na @harmonize_tz ni story ya Siku nyingine. Mungu akubariki mwanangu,” Shusho aliandika.

Harmonize kwenye chapisho hilo alimshukuru Mwimbaji huyo kwa kuwa kielelezo bora huku akimtakia Mungu kumfunika kwa damu yake.

“Amen! Inshaallah! Damu Ya YESU Ikufunike!!” Harmonize alisujudu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved