logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Waziri Kindiki aapa kukabiliana na biashara ya pombe haramu

"Isipokuwa tunafanya jambo na tukalifanya haraka tunakabiliwa na mgogoro wa vizazi.

image
na Radio Jambo

Makala01 February 2023 - 16:01

Muhtasari


  • Waziri Kindiki aliwahakikishia viongozi waliohudhuria kwamba hataacha lolote katika kuhakikisha kuwa usalama umeimarishwa katika eneo hilo

Waziri wa Usalama wa Ndani Kithure Kindiki ameapa kuzidisha vita dhidi ya visa vinavyokithiri vya utumizi wa dawa za kulevya na ukosefu wa usalama katika Kaunti ya Kiambu.

Akizungumza wakati wa hafla ya kuzindua kitengo cha Cianda huko Kiambaa Jumatano, Waziri Kindiki aliwahakikishia viongozi waliohudhuria kwamba hataacha lolote katika kuhakikisha kuwa usalama umeimarishwa katika eneo hilo.

Aliwakemea wanaojihusisha na utengenezaji wa pombe haramu na kusambaza pombe haramu katika eneo hilo huku akionya kuwa hatakubali vitendo haramu vinavyofanywa mkoani humo kwa kugharimu vizazi vijavyo.

"Kuna vitishio vitatu vya  kiusalama; ugaidi, ujambazi na pombe haramu, dawa za kulevya na utumiaji wa dawa za kulevya. Hizo ni matishio makubwa kwa usalama wa taifa letu," alisema.

"Isipokuwa tunafanya jambo na tukalifanya haraka tunakabiliwa na mgogoro wa vizazi. Hatuna uhakika wa siku zijazo. Vile vile tutakavyokabiliana na majambazi ndivyo tutakavyopambana na pombe haramu."

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved