logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kisii:Walimu sita wakamatwa kwa kuwalazimisha wanafunzi kufanya vitendo vichafu

Kulingana na OCPD, walimu hao sita wanashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Nyamache

image
na Radio Jambo

Makala01 February 2023 - 17:08

Muhtasari


  • Katika video hiyo ambayo imezua hisia mseto mitandaoni wavulana hao wadogo waliovalia sare za shule wanalazimishwa na walimu wao kufanya kitendo kichafu
Picha: KWA HISANI

Walimu sita kutoka Kaunti ya Kisii wamekamatwa kutokana na video ya kutatanisha inayosambaa kwenye mitandao ya kijamii ambapo watoto wa shule wananaswa wakionyeshwa kitendo kichafu.

Akithibitisha kukamatwa kwa walimu hao watano wa kike na mmoja wa kiume, OCPD wa Nyamache Kipkulei Kipkemboi alisema kisa hicho kilitokea katika Shule ya Msingi ya Itumbe DOK huko Nyamache.

Kulingana na polisi, sita; Everline Moraa, Gladys Kenyanya, Angelicia Joseph, Moraa Nyairo, Cathrine Mokaya na William Isoka, walikamatwa baada ya maafisa wa Wizara ya Elimu katika kaunti hiyo wakiongozwa na Mkurugenzi wa Kaunti Ndogo ya Nyamache Linet Onduso kuzuru shule hiyo baada ya kupokea klipu hiyo.

Katika video hiyo ambayo imezua hisia mseto mitandaoni wavulana hao wadogo waliovalia sare za shule wanalazimishwa na walimu wao kufanya kitendo kichafu huku wakiwa wamelala juu ya kila mmoja huku walimu wakicheka kwa sauti ya chini.

Kulingana na OCPD, walimu hao sita wanashikiliwa katika Kituo cha Polisi cha Nyamache wakisubiri kufikishwa mahakamani.

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved