logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mshukiwa wa mauaji ya wakili Willie Kimani ahukumiwa kifo

Katika uamuzi wake wa Ijumaa, Februari 3, Hakimu Jessie Lesit alimhukumu Leliman kifo

image
na Radio Jambo

Makala03 February 2023 - 08:12

Muhtasari


  • Mahakama ilisema kwamba ilizingatia kwamba Sylvia Wanjiru ndiye aliyekuwa mhusika mdogo zaidi katika kundi hilo.

Fredrick ole Leliman, afisa wa polisi ambaye alikuwa mshukiwa mkuu na ambaye alipanga mauaji ya kikatili ya Wakili Willie Kimani, mteja wake Josephat Mwenda na dereva Joseph Muiruri amehukumiwa kifo.

Maafisa  wanne, Fredrick Leliman (mshukiwa mkuu), Stephen Cheburet, na Sylvia Wanjiku, na mtoa habari Peter Ngugi, ambao walishtakiwa kwa mauaji ya wakili wa Nairobi Willie Kimani, walihukumiwa siku ya Ijumaa.

Katika uamuzi wake wa Ijumaa, Februari 3, Hakimu Jessie Lesit alimhukumu Leliman kifo huku mshtakiwa wa pili akipokea miaka 30 jela.

Mshtakiwa wa tatu, kwa upande mwingine, atatumikia kifungo cha miaka 24 jela huku mtoa taarifa wa polisi akihukumiwa miaka 20.

"Mshtakiwa wa kwanza anahukumiwa kifo katika kila moja ya makosa matatu, mshtakiwa wa pili anahukumiwa kifungo cha miaka thelathini, mshtakiwa wa tatu anahukumiwa miaka 24 na mshtakiwa wa tano anahukumiwa kifungo cha miaka ishirini," Jaji Jessie Lesit alisema.

Mahakama ilisema kwamba ilizingatia kwamba Sylvia Wanjiru ndiye aliyekuwa mdogo zaidi katika kundi hilo na alikuwa mdogo wakati wa uhalifu. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved