logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Trio Mio: Siwezi oga maji baridi!

"Nimekosa sana kuoga maji baridi shuleni, lakini siwezi oga," - Mio.

image
na Radio Jambo

Makala10 February 2023 - 07:35

Muhtasari


• Trio Mio alikamilisha masomo yake ya sekondari mwishoni mwa mwaka jana.

Trio Mio

Trio Mio, rapa mchanga Zaidi kuwahi kutokea nchini ambaye alimaliza shule mwishoni mwa mwaka jana amezungumza kile ambacho anakikosa katika maisha yake nje ya shule.

Trio Mio alifikisha miaka 18 mwaka jana, mieizi michache akisubiria kuukalia mtihani wake wa KCSE.

Kwa kawaida, watu wengi haswa wanafunzi huwa hawataki kuzungumzia kitu chochote kizuri kutoka maisha yao ya shuleni, jambo ambalo wanasema ni kama jela bila uhuru wa kufanya mambo yao. Lakini kwa Trio Mio, hali ni tofauti kwani kuna mambo mengi ameyakosa ambayo alikuwa anafurahia akiwa shuleni.

Alisema kuwa nyumbani huwa anakoga kwa maji moto lakini kama kuna kitu kikubwa anachokikosa Zaidi enzi za shuleni ni kukoga maji baridi.

“Kama kuna kitu nakosa Zaidi ni maji baridi. Siku hizi ninakoga maji moto nyumbani, namkosa mwalimu wetu mkuu, marafiki zangu na kushiriki katika burudani ya shuleni,” Trio Mio alisema.

Msanii huyo pia alifutilia mbali uwezekano wa kuendelea na masomo yake baada ya kukamiisha kidato cha nne mwishoni mwa mwaka jana.

Alisema lengo lake kuu ni kuwaunganisha vijana wenzake kupata ajira za kuwalipia bili za maishani, akidokeza tayari ameingia kwenye mtakaba wa ushirikiano na kampuni moja ya kusambaza pipi ambapo anataka vijana wajiunge ili kupewa kandarasi ya kuzunguza pipi na kupata kuzindikiza mkono kinywani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved