logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwigizaji Lenana na mkewe wafichua jinsia ya mtoto wao

Kulingana na mwigizaji huyo wanatarajia mtoto msichana.

image
na Radio Jambo

Habari01 March 2023 - 10:46

Muhtasari


  • Mapema wiki hii Lenana alifichua kwamba mkewe anamshinda katika umri huku akifichua ana miaka 34 na mkewe 36

Aliyekuwa mwigizaji wa kipindi cha Selina Lenana Kariba kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram amefichua jinsia ya mtoto wake.

Kulingana na mwigizaji huyo wanatarajia mtoto msichana.

Lenana na mkewe walifichua kuwa wanatarajia mtoto wao wa kwanza mapema wiki hii.

Lenana alisema;

Wikendi iliyopita familia yangu iliandaa baby shower ya ajabu kwa ajili yetu kusherehekea hatimaye kuwa na msichana mwingine kujiunga na genge (we are such a boy family 😂)... tulikuwa na wakati mzuri wa kusherehekea na wale wa karibu zaidi 🩷,"Aliandika Lenana.

Mapema wiki hii Lenana alifichua kwamba mkewe anamshinda katika umri huku akifichua ana miaka 34 na mkewe 36.

Mashabiki waliwapongeza wawili hao na hizi hapa baadhi ya jumbe zao;

anitanderu: Hongereni Honey Buns!!! nawafurahia wote  wasicha ni watoto wa ajabu❤️❤️❤️❤️

shikshaarora: Malkia mrembo zaidi anakuja, hongereni!!!!

mpweety_cortez: Timu wasichana, atakuwa mrembo zaidi 😍

gloshygyal: So both Patricia Mackenzie's sons wameamua to premier with girls. Nice! As a mother of 3 sons only this post has tickled my ovaries😊

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved