logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Najua mtaniombea kifo-Amber Ray asema baada ya kulazwa hospitali

Alinukuu picha kwa kusema kuwa maadui zake na watu wa kijiji ndio chanzo kikuu.

image
na Radio Jambo

Habari03 March 2023 - 14:04

Muhtasari


  • Amber aliendelea kusema kuwa daktari alimwambia kuwa ana maambukizi ya damu lakini daktari alimhakikishia kuwa mtoto yuko sawa

Mwanasosholaiti Faith Makau almaarufu  Amber Ray amelazwa hospitalini.

Amber kupitia ukurasa wake wa  Instagram alipakia ideo akiwa kwenye kitanda cha hospitali.

Alinukuu picha kwa kusema kuwa maadui zake na watu wa kijiji ndio chanzo kikuu.

Amber aliendelea kusema kuwa daktari alimwambia kuwa ana maambukizi ya damu lakini daktari alimhakikishia kuwa mtoto yuko sawa.

Aliendelea kuwaambia watu wa kijiji chake na maadui wasimfanyie mazoezi.

Amber aliandika hivi,

"Watu wa kijiji changu na maadui wamejaribu moyo wangu wakapata ni mawe. Sasa wameona ugongwa ndo utaniweza. Anyway daktari amesema ni maambukizi ya damu lakini mtoto yuko sawa, na tafadhali msiniombee coz najua wengi wenu mtaniombea kifo. Ila nimelindwa na Mungu. ."

Haya yanajiri siku chache baada ya mpenziwe kuweka wazi kwamba wawili hao hawajaachana,ila wamekuwa wakipitia misukosuko kwenye uhusiano kama uhusiano mwinginewowote.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved