logo

NOW ON AIR

Listen in Live

DJ wa Tanzania acheza mziki juu ya mlima Kilimanjaro

Joozey ni mmoja wa wanamuziki wanaochipuka Tanzania.

image
na Radio Jambo

Makala06 March 2023 - 07:26

Muhtasari


• DJ Joozey alicheza muziki wa dakika kumi na tano katika kilele cha mlima huo wenye urefu wa mita 5895

Dj mmoja wa Tanzania amewashangaza watumiaji wa mtandao baada ya kusambaza video ambayo alikuwa akicheza muziki kwenye kilele cha mlima mrefu zaidi Afrika, Mlima Kilimanjaro.

Joseph Simo anayejulikana kwa jina maarufu kama DJ Joozey alicheza muziki wa dakika kumi na tano katika kilele cha mlima huo wenye urefu wa mita 5895

" Mimi ni mwanamume wa kwanza kuwahi kucheza seti ya DJ ya dakika 15. MUNGU NI MWEMA!” DJ alinukuu kipande cha video yake juu ya Mlima Kliimanjaro .

Joozey ni mmoja wa wanamuziki wanaochipuka Tanzania.

Kulingana na jarida la Tangaza Magazine, kijana huyo mwenye umri wa miaka 27 amekuwa kwenye tasnia ya showbiz kwa takriban miaka mitano.

Mwaka jana, DJ huyo alikuwa mmoja wa Waafrika wachache waliochaguliwa kushiriki katika kampeni ya albamu ya rapa wa Marekani DJ Khaled kwa ajili ya albamu yake ya ‘God Did’.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved